KINYOZI ADAIWA KUMBAKA MTOTO WA MIAKA 13 AMBAYE NI HAUSIGELI MKOANI KILIMANJARO

WIMBI la watoto waliochini ya umri wa miaka kumi na nane, kufanyiwa ukatili wa kubakwa, kulawitiwa na kutumikishwa adhabu mbalimbali linazidi kushika kasi nchini hususani katika mkoa wa Kilimanajaro ambapo matukio hayo yamezidi kushika kasi na katika kipindi cha wiki tatu matukio matatu hayo yameutikisa mkoa huo yakihusisha watoto walio katika umri mdogo. 

Aidha, Mtoto mwingine mwenye umri wa miaka kumi na tatu mfanyakazi wa ndani na mkazi wa Majengo Wilayani Moshi, mkoani humo amebakwa na kuumizwa vibaya katika sehemu za siri na, Rajabu Hamza(18), Kinyozi mkazi wa Njoro. 

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani humo, Koka Moita, amesema kuwa tukio hilo lilitokea Juni 12, 2014 saa moja jioni katika mtaa wa Majengo Wilayani Moshi, baada ya Rajabu, kumshawishi msichana huyo kuwa amfuate katika nyumbani aliyopanga rafiki wa mtuhumiwa 'geto' ndipo alipoamua kumbaka wakati akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria. 

“Kwa sasa tunashindwa kuelewa ni kwanini matukio ya ubakaji kwa hawa watoto wa kike yameshika kasi kipindi hiki, kwani itakumbukwa ndani ya wiki karibia tatu wameshabakwa watoto watatu, ambapo wawili kati ya hao wamebakwa na baba zao wazazi” alisema Moita. 

Amesema kuwa Jeshi la polisi mkoani humo linamshikilia mtuhumiwa huyo kwa mahojiano zaidi na pindi ushahidi utakapo kamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani. 

Amewataka wazazi na walezi, kuwa makini na uangalizi mkubwa kwa watoto wao, na kuepuka kuwaachia ovyo watoto wao kwa watu mbalimbali na kuwa na ukaribu na watoto hao. 

Katika tukio jingine mtu mmoja amekufa kwa kujinyonga ndani ya chumba chake katika kijiji cha Kiboroloni-Makao mapya Wilayani Moshi, mkoani humo. 

Moita, amesema tukio hilo lilitokea Juni 12, 2014 saa 12:00 mchana na kumtaja marehemu kuwa ni, Izaki John (30).

“Tulimkuta akiwa amejinyonga kwa kutumia Mkanda wake wa suruali na alikuwa ameshakufa, ndipo Polisi wetu walimtoa na kumchukua kwa ajili ya uchunguzi" alisema Moita. 

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya mkoa ya Mawezi, kwa uchunguzi zaidi, huku Jeshi la hilo likiendelea na upelelezi ili kujua chanzo cha marehemu kuamua kujinyonga. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo