ASKARI HUYU WA USALAMA BARABARANI ALAZIMIKA KUHATARISHA MAISHA YAKE UBUNGO MATAA, SHUHUDIA MWENYEWE

Tukio la aina yake ambalo limeonekana kuwashangaza wengi limetokea kwenye mataa ya kuongozea magari jijini dar es Salaam ambapo askari wa usalama barabarani ameamua kusimama mbele ya magari yaliyokaidi amri yake ya kuzuia magari ya upande huo yasipite kwanza

Tukio hilo limetokea mwishoni mwa wiki ambapo askari huyo ambaye jinalake halikupatikana mara moja aliamua kuyazuia magari mawili toyota baloon yaliyokaidi amri yake aliyoitoa kuwa magari ya upande huo yasimame ili aite magari ya upande mwingine
Wakati askari huyo alipotoa amri ya kuzuia magari yaliyokuwa yakitoka mjini kwenda mbezi na maeneo mengine ya nje ya mji, aligeuka upande wa pili kuita mengine lakini ghafla madereva hao wakataka kutumia mwanya huo wa kugeuka kwa askari kupenya

Jambo hilo lilionekana kumkera askari huyo ambaye alitoa ishara ya kuzuia magari yote kupita kwa muda halafu akasimama mbele ya magari hayo yaliyotaka kupita kwa nguvu huku akiwaambia kama wao ni madereva wamgonge wapite
Kitendo hicho kilichochukua zaidi ya dakika 5 kilionekana kuwashangaza wengi na pia madereva hao walishindwa kupita na kulazimika kutii amri ya polisi huyo ya kuwataka warudishe magari yao nyuma na kusubiri kwenye foleni hadi hapo upande wao utakapoitwa


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo