Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Katavi ACP Dhahiri Kidavashari
******
******
Tukio
hilo limetokea usiku wa kuamkia jana baada ya mtuhumiwa kurudi nyumbani
akitokea kwenye Sherehe ya Komonio akiwa amelewa na kuanza kuwapiga
watoto wake kwa fimbo hadi wakazirai.
Akizungumzia
tukio hilo, Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani humo, Frednandi Rwegasila,
alisema mtuhumiwa alikuwa akiishi na watoto muda mrefu baada ya kuachana
na mkewe.
Aliwataja
watoto hao kuwa ni Daniel Paskali (11) ambaye ndiye aliyefariki na
Jackson Paskali (9) ambao baada ya kuzirai kwa kipigo na mtuhumiwa
kukimbia, majirani walikwenda kutoa msaada wa kuwapeleka hospitali.
"Wakiwa
njiani, Daniel alifariki dunia wakati Jackson amelazwa katika Hospitali
ya Mkoa akiendelea kupatiwa matibabu na ameumizwa sehemu mbalimbali ya
mwili wake," alisema.
Kamanda Rwegasila alisema jeshi hilo linaendelea kumsaka mtuhumiwa ili aweze kufikishwa mahakamani.