MTOTO WA MWAKA MMOJA AFARIKI BAADA YA KUTUMBUKIA KWENYE NDOO YA MAJI



MTOTO wa umri wa mwaka mmoja amekufa baada ya kutumbukia kwenye ndoo ya maji nyumbani kwao, wakati akicheza.
 
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Kihenya wa Kihenya, tukio hilo ni la juzi saa 4:30 asubuhi katika eneo la Buza.
 
Alisema mtoto huyo, Najma Omary alikuwa akicheza nje ya nyumba yao kulikokuwa na ndoo ya maji na alitumbukia kwa kutanguliza kichwa na kunywa maji mengi yaliyosababisha mauti yake.
 
Kamanda Kihenya alisema maiti ya mtoto huyo imehifadhiwa hospitali ya Temeke na hakuna mtu anayeshikiliwa na Polisi na kwamba uchunguzi zaidi wa tukio hilo unaendelea kufanywa.
 
Katika tukio la pili, watu 14 wamekamatwa na polisi katika mikoa miwili tofauti ya kipolisi kwa tuhuma za kukutwa na pombe haramu ya gongo pamoja na misokoto ya bangi.
 
Kamanda Kihenya alisema Polisi waliendesha msako juzi asubuhi maeneo ya Kingungi kwa Nyoka, huko Kiburugwa na kuwakamata watu tisa wakiwa na bangi puri moja na kete 92. 

Watuhumiwa hao wanashikiliwa na watafikishwa mahakamani.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo