Mauaji ya kinyama yametikisha Mkoa wa Mwanza baada ya
miili ya wanaume watatu ambao majina yao hayajafahamika wala makazi yao,
kukutwa imefichwa kwenye vichaka vilivyopo kitongoji cha Kijinga
Kijiji cha Igaka wilayani hapa Mkoa wa Mwanza.
Miili hiyo ilikutwa jana asubuhi kwenye vichaka hivyo baada ya kuuawa kwa kipigo na kunyongwa shingo na watu wasiofahamika usiku wa kuamkia jana.
Inadhaniwa kuwa huenda walikuwa ni wafanyabiashara wa ng'ombe au wezi kutokana na mauaji yao kufanyika usiku wa kuamkia siku ya mnada wa ng'ombe kwenye kijiji jirani cha Sima kilichopo wilayani hapa.
''Miili yao imeharibiwa kwa kipigo na ina majeraha kiasi cha kuharibika lakini bado inaweza kutambuliwa.... inawezekana wapo wanaoweza kuwafahamu lakini wanasita maana bado haijafahamika wameuawa katika mazingira gani, '' amedai mmoja wa watu walioshuhudia miili hiyo wakati akizungumza na NIPASHE mnadani hapo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Valentino Mlolowa alithibitisha miili hiyo kukutwa katika vichaka vilivyopo kwenye kitongoji hicho kilichopo mpakani mwa Wilaya ya Sengerema na Geita.
Mlolowa alisema miili hiyo imehifadhiwa katika hospitali teule ya Wilaya ya Sengerema baada ya juhudi za kuitembeza baadhi ya maeneo yenye mikusanyiko ya watu yakiwamo ya kwenye mnada huo wa Sima, Soko Kuu na kituo cha mabasi Sengerema kutotambuliwa.
Alisema inaonyesha kuwa huenda watu hao waliuawa katika eneo jingine na kutupwa kwenye vichaka hivyo.
Kamanda huyo alisisitiza kuwa bado wanaendelea kufanya uchunguzi ili kuwabaini watu hao waliouawa, sababu za mauaji na wauaji wao.
Miili hiyo ilikutwa jana asubuhi kwenye vichaka hivyo baada ya kuuawa kwa kipigo na kunyongwa shingo na watu wasiofahamika usiku wa kuamkia jana.
Inadhaniwa kuwa huenda walikuwa ni wafanyabiashara wa ng'ombe au wezi kutokana na mauaji yao kufanyika usiku wa kuamkia siku ya mnada wa ng'ombe kwenye kijiji jirani cha Sima kilichopo wilayani hapa.
''Miili yao imeharibiwa kwa kipigo na ina majeraha kiasi cha kuharibika lakini bado inaweza kutambuliwa.... inawezekana wapo wanaoweza kuwafahamu lakini wanasita maana bado haijafahamika wameuawa katika mazingira gani, '' amedai mmoja wa watu walioshuhudia miili hiyo wakati akizungumza na NIPASHE mnadani hapo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Valentino Mlolowa alithibitisha miili hiyo kukutwa katika vichaka vilivyopo kwenye kitongoji hicho kilichopo mpakani mwa Wilaya ya Sengerema na Geita.
Mlolowa alisema miili hiyo imehifadhiwa katika hospitali teule ya Wilaya ya Sengerema baada ya juhudi za kuitembeza baadhi ya maeneo yenye mikusanyiko ya watu yakiwamo ya kwenye mnada huo wa Sima, Soko Kuu na kituo cha mabasi Sengerema kutotambuliwa.
Alisema inaonyesha kuwa huenda watu hao waliuawa katika eneo jingine na kutupwa kwenye vichaka hivyo.
Kamanda huyo alisisitiza kuwa bado wanaendelea kufanya uchunguzi ili kuwabaini watu hao waliouawa, sababu za mauaji na wauaji wao.
CHANZO:NIPASHE