WAENDESHA BODABODA MWANZA WAASWA KUACHA UHALIFU

Kamishna wa Polisi Jamii Tanzania Mussa Ali Mussa, amewataka wafanyabiashara wadogo (Machinga) na Bodaboda Jijini Mwanza kutokubali kutumiwa na baadhi ya makundi ya watu wanao jihusisha na uhalifu.

Mwezi Mei 27 katika eneo la Makoroboi, Kamishina Ali, alieleza kwamba, yapo baadhi ya makundi ya wahalifu ambayo hayana nia njema kwa watanzania badala yake yanakuwepo kwa ajili ya kuwakosesha amani wananchi na kusababisha vurugu zisizo na manufaa yoyote katika jamii.

“Baadhi ya makundi kazi yake ni uhalifu, hivyo msikubali kutumiwa na hayo makundi kwani hayana nia njema na sisi kutokana na kuona kuwa tuna kipato kidogo na endapo tukijihusisha nao tutajitoa katika dhima njema tuliyo kusudia”, alisema Kamishina .

Alieleza kwamba kutokana na makundi hayo ya Machinga na Bodaboda, kuna uwezekano mkubwa wa watu waovu kujiingiza katikati yao na kuwataka kuwapa pesa katika kuwabaini watu hao mapema iwezekanavyo.

“Bodaboda nyingi hutumiwa na wahalifu kwa ajili ya wizi, cha msingi ni kuwatambua mapema ili msijiharibie sifa zenu za uendeshaji kwani jeshi la polisi lina mkakati wa kuwawekea mazingira safi ya kazi ili kuepukana na ajali za mara kwa mara”, alieleza.

Kamishina Ali, alikabidhi pikipiki 13 zenye thamani ya sh.milion mbili, ambazo zilipatikana kutoka kwa madereva pikipiki wa kituo cha Tanesco ambao walikuwa wakichangia sh. 5,000 kila siku kwa kila mmoja na hivyo kujipatia pikipiki hizo ambazo ni msaada mkubwa kwao katika utendaji wa kazi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo