KUNDI LA MBWA WENYE KICHAA LAIBUKA NA KUNG'ATA WATU MKOANI DODOMA

Kundi la mbwa wenye kichaa limezuka katika Mtaa wa Swaswa  Manispaa ya Dodoma na kusababisha hali ya taharuki  baada ya kuwangata watu wawili na kuwasasabishia maamuvu makali. 
  Akizungumza nasi mzazi wa  mmoja wa mtoto  alieng’atwa na mbwa hao Bw  Jonathani Ngossi amesema  kuwa mbwa hao wamekuwa wakiwang’ata watu wazima na watoto hivyo kupelekea  kutibiwa kwa gharama kubwa.
  Aidha Bw Ngossi imeitaka serikali kwenda kutoa chanjo kwa mbwa hao ili kupunguza  tatizo hilo na kama ikishindikana  iwapige risasi  mbwa hao.
  Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtaa huo Bw Chales Nyuma amekiri kuwepo kwa  tatizo hilo na kusema kuwa mpaka sasa watu wawili pamoja na kuku wawili wameshang’atwa na mbwa hao na wanaendelea kutishia amani mtaani hapo
  Sanjari na hayo Bwana Nyuma   ameongezea kuwa  kwa baadae  wanakusudia kutoa elimu  kwa watu wenye mbwa juu ya  taratibu za kuwafuga.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo