BEKI AVUNJA MKATABA NA KUTUA YANGA

Na Martha Mboma. BEKI wa Coastal Union, Abdi Banda, amefunguka  na kusema yupo katika hatua nzuri ya kuweza kumalizana na Yanga, huku akiwa anavunja mkataba wake.
 
Beki wa Coastal Union, Abdi Banda.

Kabla ya msimu uliopita Yanga ilikuwa ikimhitaji beki huyo ambaye alipandishwa kutoka timu ya vijana ya Coastal na kuweza kuchezea timu kubwa lakini aliwatolea nje.

Akizungumza na Championi Jumatano, beki huyo alisema kwa sasa yuko katika mazungumzo mazuri na Yanga kwa ajili ya kuungana nao kwa msimu ujao na anavunja mkataba na timu yake.

Banda alisema ameamua kujiungana na timu nyingine na anatarajia kuvunja mkataba na Coastal japo sababu za kuvunja hajaziweka wazi na kukiri kuwa mazungumzo yapo katika hatua nzuri.
 
“Kwa sasa nipo katika mazungumzo na Yanga na tumefika pazuri, suala la kuendelea kuitumikia Coastal Union halipo kwa sababu  natarajia kuvunja nao mkataba ili niweze kuendelea na mambo yangu.

“Yanga walikuwa wakinihitaji kwa muda mrefu lakini tukikubaliana na tumefika pazuri, nipo tayari kwenda kuitumikia na si kurudi Coastal ingawa sipo tayari kusema ni kitu gani kimenifanya niondoke kule,” alisema Banda.

Japo kwa upande wa Coastal Union hali si shwari kumekuwa na migogoro baina ya viongozi huku wachezaji wengi wakiripotiwa  kuondoka na hata kuvunja mikataba yao kutokana na kutokuwepo  kwa maelewano mazuri ndani ya klabu.

>>>Championi Jumatano


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo