WATU WAWILI WAFARIKI DUNIA KWA KUJINYONGA WILAYANI MAKETE

Watu wawili wamefariki dunia kwa kujinyonga katika matukio yaliyotokea nyakati tofauti wilayani Makete mkoani Njombe huku matukio hayo yakishabihiana kwa kiasi fulani

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na ofisi ya mkuu wa polisi wilayani Makete hii leo imesema katika tukio la kwanza Bi Anamaria Mahenge aligundua kujinyonga hadi kufa kwa Paul Mbilinyi ambaye alijinyonga kwa kutumia kitambaa cha wanawake cha kujifungia Kichwani

Tukio hilo limetokea Aprili 30 mwaka huu majira ya saa mbili asubuhi katika kijiji cha Ivalalila kata ya Iwawa wilayani hapa

Aidha taarifa hiyo imesema katika tukio la pili jeshi hilo lilipokea taarifa ya kujinyonga hadi kufa kwa Fonzina Israel Msigwa ambaye naye alijinyonga kwa kutumia kitambaa cha kujifunga kichwani cha wanawake

Tukio hilo lilitokea Mei 4 mwaka huu majira ya saa tano kamili usiku huko katika kijiji cha Ibaga kata ya Mang'oto wilayani hapa

Matukio hayo licha ya kutokea katika vijiji tofauti yanafanana kwani wote waliofariki walijinyonga kwa kutumia kitambaa cha kujifunga kichwani cha wanawake.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo