WAFANYAKAZI WALIOTIMULIWA MBEYA WASHINDA KESI

Na Kenneth Ngelesi

JUMLA ya kesi 21 zinazohusiana na matatizo ya  wafanyakazi sehemu za kazi, zimefunguliwa na baadhi yake kutolewa uamuzi katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Akizungumza  hivi karibuni, Katibu wa Shirikisho la Vyama Huru vya Wafanyakazi (TUCTA) mkoani Mbeya, William Mboma, alisema kuwa kesi hizo zinahusu nia za malalamiko mbalimbali ya wafanyakazi ikiwa ni pamoja na kuachishwa kazi kinyume cha taratibu.

Mbona alisema kuwa kati ya kesi hizo, 12 zimeshatolewa uamuzi na wafanyakazi husika wamerejeshwa kazini kwa mujibu wa sheria katika kipindi cha kuanzia Mei mwaka jana hadi sasa.

Hata hivyo, alisema kesi hizo zipo nyingi na zimeendelea kushughulikiwa taratibu kutokana na upungufu wa watumishi waliopo katika mamlaka zinazoshughulikia kesi hizo ambazo ni Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA).

Shirikisho la Vyama Huru vya Wafanyakazi nchini lina vyama 13 wanachama, ingawa si kila chama kina wanachama katika kila mkoa, jambo ambalo amesema linatokana na baadhi ya wafanyakazi kutojua umuhimu pamoja na haki zao za kisheria juu ya vyama hivyo.

Mboma alisema moja ya sababu zinazochangia kucheleweshwa kwa kesi hizo ni upungufu wa watumishi katika mahakama hizo.

Kuhusu maadhimisho ya Sikukuu ya Wafanyakazi (Mei Mosi), Mboma alisema kitaifa itaadhimishwa jijini Dar es Salaam na kaulimbiu yake ni ‘Utawala bora utumike kutatua kero za wafanyakazi’.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo