POLISI AIBIWA PIKIPIKI UWANJA WA TAIFA

KATIKA hali ya kushangaza na kusikitisha, askari polisi Raphael Maganga, juzi aliibiwa pikipiki yake aliyokuwa ameiegesha ndani ya Uwanja wa Taifa wakati wa mechi ya kirafiki kati ya Taifa Stars na Burundi.

Mechi hiyo ya kirafiki iliyomalizika kwa Stars kukubali kichapo cha mabao 3-0, ilitazamwa na mashabiki bure baada ya kudaiwa Rais Jakaya Kikwete aliamuru waingie bure ili waipe sapoti timu hiyo.

Akizungumza kwa masikitiko mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Maganga akiwa ameshika funguo zake mkononi, alisema haamini kilichotokea, kwani anaona kama ‘movie’.

Maganga alisema pikipiki yake yenye namba za usajili T 454 CUP, aina ya Fekon, aliipaki upande wa kulia wa uwanja na baada ya mechi kumalizika hakuikuta.

Alisema ameshafungua jalada lenye namba CHA/RB/36665/2014 Kituo cha Polisi Chang’ombe.

Na Clezencia Tryphone


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo