HAMISA MOBETO ALIKANA PENZI LA DIAMOND PLATNUMZ



Mrembo aliyewahi kushiriki miss Tanzania Hamisa Mobeto a.k.a Hamisa kadomo amekanusha tetesi za kuwa na uhusiano wa kimapenzi na msanii kipenzi cha kinadada Naseeb Abdul a.k.a Daimond Platnumz na kusema kuwa anamuheshimu kama shemeji yake.
 
Hamisa ambaye pia amewahi kuonekana katika video ya msanii Quick Rocka ‘My baby’, ameiambia Global Publishers kuwa maneno yanayosemwa  si ya kweli na wala haitawahi kutokea.

“Kamwe siwezi kutembea na Diamond na haitatokea kwani jamii nzima inajua yupo na Wema na mimi huyo mtu ni rafiki yangu mkubwa, hana chake hapa, siwezi kutembea naye kamwe, namheshimu kama shemeji yangu”.Alisema mrembo huyo.
 
Mrembo huyo ambaye uzuri wake unazidi kumpa dili kibao ndani na nje ya Tanzania kila kukicha, ameongeza kuwa hana mazoea na staa huyo wa ‘Number One’ na kama kuonana waliwahi kuonana miaka ya nyuma na si kimapenzi.
 
Source: Global Publishers


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo