WANAUME AMBAO HAWAJAFANYIWA TOHARA IRINGA,WATAKIWA KUACHA KUWA NA AIBU,BADALA YAKE WAJITOKEZE KWENYE VITUO VYA AFYA


Baadhi ya Wananchi ambao hawajafanyiwa tohara, wametakiwa kuacha aibu na kujitokeza  kwenye vituo vya afya ili kuweza kupata huduma hiyo na kuacha  kukwepa kupata huduma katika vituo vyao ambavyo wamevizoea.

Hayo yamesemwa na meneja wa Mradi wa tohara mkoa wa iringa Dr.Abdalah Maganga, na kusema kuwa watu kuanzia umri wa miaka 25 kwenda juu wamekuwa hawajitokezi kupatiwa huduma hiyo kutokana na kuwa na aibu.

Dr.Abdalah  amesema kuwa asilimia kubwa ya watu wanaojitokeza kupata huduma hiyo ni wale wenye umri wa miaka 18 kushuka chini ,huku sababu kubwa akitaja kuwa ni kuhofia kukaa muda mrefu bila kufanya mapenzi kwa kipindi cha wiki sita wakati akisubiri kidonda kupona.

Hata hivyo ametaja sababu kubwa kuwa wengi wao hawapendi kufanyiwa tohara na wanawake kutokana na kuwa idadi kubwa ya wahudumu ni wanawake.

Amesema kuwa katika kampeni iliyofanyika katika kipindi cha wiki nne iliyolenga wilaya tatu imekuwa na mafanikio ambapo mpango wao ilikuwa ni kuwafikia WATU 15 elfu lakini wamefikia watu 16 elfu na 200 .

Aidha ameongeza kuwa  kuanzia tarehe 10 februali had 8 mach wataanza kampeni katika wilaya za mkoa wa Njombe na lengo ni kuwafikia watu 15 elfu huku akiahidi kurudia maeneo ambayo hawakuyafikia katika wilaya, ambazo tayari wamefanya kampeni ambazo ni kilolo,iringa vijijini,na mufindi kwa wiki mbili.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo