WANAFUNZI WANNE WAFARIKI DUNIA KWA KUGONGWA GARI WAKATI WAKIKIMBIA MCHAKAMCHAKA...!!

Habari zilizoufikia  zinasema kuwa Wanafunzi wanne Wa shule ya sekondari Mustapha Sabodo iliyopo mjini Mtwara wamekufa na wengine zaidi ya 20 kujeruhiwa baada ya kugongwa na gari aina ya Benz wakiwa kwenye mchakamchaka asubuhi ya leo.

Tukio hilo limetokea leo asubuhi wakati wanafunzi hao wakikimbia mchaka mchaka.....

Chanzo cha ajali hiyo kinatokana na gari dogo aina ya Benzi kumgonga mwanafunzi mmoja aliyekuwa kwenye mchakamchaka na katika hali ya taharuki ya mwenzao bila kuangalia nyuma ndipo lori  jingine likawagonga wanafunzi wengine na kusababisha mwanafunzi mmoja kufariki dunia papo hapo na wengine watatu wakifariki hospitali wakati wakipatiwa matibabu huku wengine 20 wakiwa wamejeruhiwa.

Dreva wa Benzi amejisalimisha kituo cha polisi Mtwara lakini Yule wa Lori amekimbia.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo