PIGO TASNIA YA HABARI: MWANAHABARI TRYPHON MPILUKA AFARIKI DUNIA KWA KUGONGWA NA GARI

 
Marehemu Tryphone Mpiluka enzi za uhai wake akitangaza redio Kitulo FM

Tasnia ya habari imepata pigo baada ya mwanahabari aliyekuwa akiendelea na masomo yake ya uandishi wa habari Bw. Tryphone Mpiluka kufariki dunia ghafla usiku wa kuamkia leo kwa ajali

Taarifa za awali zinasema Marehemu Tryphone amepoteza maisha baada ya kugongwa na gari wakati akisafiri kuelekea shambani kwa kutumia baiskeli hali iliyopelekea kifo chake huko Nyololo wilaya ya Mufindi mkoani Iringa

Enzi za uhai wake marehemu alifahamika sana nyanda za juu kusini hasa wilayani Makete na maeneo ya jirani wakati akifanya mazoezi ya utangazaji katika kituo cha redio Kitulo FM kinachomilikiwa na halmashauri ya wilaya ya Makete

Kutokana na umahiri wake wa kutangaza marehemu aliamua kuendelea zaidi na masomo ambapo hadi mauti yanamkuta alikuwa akisoma masomo ya uandishi wa habari na utangazaji katika chuo cha Royal College Of Tanzania

Mungu aiweke roho ya marehemu Tryphone Mpiluka mahali pema peponi Amen 

zifuatazo ni baadhi ya picha za marehemu enzi za uhai wake




JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo