SOKO LA KIMATAIFA KUJENGWA MAKAMBAKO NJOMBE

Kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Makambako Bi.Tina Sekambo Akiwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Hiyo Bwana Chesco Hanana Mfikwa.

Baadhi ya Madiwani wa Kata za Halmashauri ya Mji wa Makambako Wakifuatilia Kwa Makini Elimu ya Ujenzi wa Soko la Kimataifa Kwenye Halmashauri Ya Mji wa Makambako Mkoani Njombe.

Na Gabriel  Kilamlya MAKAMBAKO
Halmashauri ya Mji wa Makambako Kwa Kushirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara Wanatarajia Kujenga Soko la Kimataifa Katika Mji wa Makambako.

Soko Hilo Limetajwa Kujumuisha Huduma Mbalimbali za Kijamii Ikiwemo Sehemu za Hoteli, Maegesho ya Magari Makubwa ya Mizigo na Madogo,Huduma za Vinywaji vya Aina Mbalimbali Hali Itakayochangia Kupatikana Kwa Ajira Nyingi Zaidi.

Akizungumza Mara Baada ya Kikao cha Baraza la Madiwani Katika Halmashauri Mji wa Makambako Kilichofanyika Januari 24 Mwaka Huu Afisa Ardhi Kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi Tanzania Profesa Aldo Lupala Amesema Hatua za Usanifu Pamoja na
Mchoro wa Soko Hilo Tayari Zimeshakamilika na Kubaini Changamoto Mbalimbali  Ikiwemo Kubaini Kaya 76 Zitakazo Lipwa Fidia.

Kwa Upande Wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Makambako  Chesco Hanana Mfikwa Amewaomba Wadau Mbalimbali Kujitokeza Kuwekeza Katika Ujenzi wa Soko Hilo Kwani Kama Serikali Imeiachia Halmashauri Kujenga Soko Hilo Kwa Asilimia Kubwa.

Pamoja na Mambo Mengine Amewataka Wakazi wa Eneo Litakalojengwa Soko Hilo Mtaa wa Mashujaa Kata ya Mji Mwema Makambako Kuacha Kusogeza Shuguli za Ujenzi Katika Eneo Hilo Kwani Watakao Lipwa Fidia ni Wale Waliokutwa Wakati wa Upembuzi Yakinifu Ambao Watalipwa Zaidi ya Shilingi Bilioni 2,


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo