
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbrod
Slaa, amesema ili nchi iondokane na hali ya umaskini, wananchi
wanatakiwa kufanya uamuzi mgumu wa kutoirudisha CCM madarakani, katika
uchaguzi mkuu ujao, utakaofanyika mwakani.
Dk. Slaa alisema misingi mibovu ya CCM ndiyo sababu ya nchi kuyumba na kwamba hali hiyo imechangia Tanzania kuwa ya pili kutoka mwisho kwa umaskini barani Afrika, wakati nchi ipo katika nafasi ya pili kwa kuwa na rasilimali nyingi.
Kauli hiyo aliitoa wakati akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Siasa, katika Wilaya ya Kyela, mkoani Mbeya, ikiwa ni mwendelezo wa Operesheni M4C Pamoja Daima.
Alisema, endapo wananchi watakubali kuwa na uamuzi mgumu katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu ikifika 2015 kwa kuipa Chadema nafasi ya kuongoza nchi, basi watambue kuwa wameondokana na hali hiyo ya umaskini.
“Kitu cha kwanza kukifanya pindi tutakapoingia Ikulu 2015 ni kuuza ndege ya Rais pamoja na mashangingi ya wabunge, ili fedha itakayopatikana tuipeleke kwenye shughuli za maendeleo,” alisema.
Dk. Slaa aliwapongeza wananchi kwa kutoa maoni yao ambapo wananchi milioni 3 na laki 3 walitoa maoni yao, huku asilimia 72 wakitaka ardhi ya Tanzania wamiliki wenyewe.
Dk. Slaa alisema misingi mibovu ya CCM ndiyo sababu ya nchi kuyumba na kwamba hali hiyo imechangia Tanzania kuwa ya pili kutoka mwisho kwa umaskini barani Afrika, wakati nchi ipo katika nafasi ya pili kwa kuwa na rasilimali nyingi.
Kauli hiyo aliitoa wakati akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Siasa, katika Wilaya ya Kyela, mkoani Mbeya, ikiwa ni mwendelezo wa Operesheni M4C Pamoja Daima.
Alisema, endapo wananchi watakubali kuwa na uamuzi mgumu katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu ikifika 2015 kwa kuipa Chadema nafasi ya kuongoza nchi, basi watambue kuwa wameondokana na hali hiyo ya umaskini.
“Kitu cha kwanza kukifanya pindi tutakapoingia Ikulu 2015 ni kuuza ndege ya Rais pamoja na mashangingi ya wabunge, ili fedha itakayopatikana tuipeleke kwenye shughuli za maendeleo,” alisema.
Dk. Slaa aliwapongeza wananchi kwa kutoa maoni yao ambapo wananchi milioni 3 na laki 3 walitoa maoni yao, huku asilimia 72 wakitaka ardhi ya Tanzania wamiliki wenyewe.