Martha Mboma na Musa Mateja
MSHAMBULIAJI wa Azam FC, Gaudence Mwaikimba, amefanikiwa kupiga hatua baada ya hivi karibuni kununua gari aina ya Toyota Brevis lenye thamani ya shilingi milioni 18.
MSHAMBULIAJI wa Azam FC, Gaudence Mwaikimba, amefanikiwa kupiga hatua baada ya hivi karibuni kununua gari aina ya Toyota Brevis lenye thamani ya shilingi milioni 18.
Championi lilimshuhudia Mwaikimba aliyewahi
kukipiga Yanga miaka ya nyuma akiwa na ndinga yake hiyo alipokuwa
akihudhuria kwenye mazoezi ya timu hiyo yanayofanyika kwenye Uwanja wa
Chamazi, Dar, juzi.
Mwaikimba anayesadikika kuwa mrefu kuliko wachezaji wengine klabuni
hapo, alisema kuwa aliupenda muundo wa gari hilo ulivyo ndiyo maana
akaamua kulinunua kwa ajili ya matumizi yake na familia.
“Nafurahi na najivunia kuwa na aina ya gari hii ya Brevis kwa sababu ni matunda ya kazi yangu na nimenunua shilingi milioni 18, kujituma kwangu na kujiwajibisha kumenisaidia sana kufikia hapa nilipo.
“Japo si gari yangu ya kwanza kumiliki, nilishawahi kumiliki magari
ya aina tofauti sana na baada ya kuwa namiliki ile Baloon ya kipindi
kile ambacho nilikuwa nacheza Yanga, niliiuza na kununua nyingine, japo
ilikuwa inapendwa na wengi kutokana na mbwembwe zake lakini kwa sasa
ndiyo namiliki hii Brevis,” alisema Mwaikimba.
VIA GPL
