Wanaume wanne wanaoshukiwa kuhusika katika shambulio la Westgate wakiwa kortini Nairobi Novemba 4, 2013. Picha/PAUL WAWERU
Na RICHARD MUNGUTI
WASHUKIWA wanne wa
ugaidi wanaohusishwa na shambulizi la duka la Westgate Septemba 21
ambapo watu 67 walikufa Jumatano walinyimwa dhamana.
Hakimu mkuu
katika mahakama ya milimani Nairobi Bw Kiarie Waweru Kiarie alisema
“washukiwa hao ni hatari na wakiachiliwa watatoroka.”
Bw Kiarie aliamuru serikali iwasilishe ushahidi katika kesi hiyo ndipo washukiwa wajue hatma yao.
“Nakubaliana
na upande wa mashtaka kwamba kesi inayowakabili washtakiwa ni mbaya na
adhabu yake ni kali. Wakiachiliwa kwa dhamana wakati huu huenda wasifike
kortini tena wakati wa kusikizwa kwa kesi,”akasema Bw Kiarie.
Alikubaliana
na wakili wa Serikali Bw Warui Mungai kwamba “ baadhi ya washtakiwa hao
hawana makao maalum na wakiachiliwa mahakama haijui kule inaweza
kuwapata wakikosa kufika kortini.”
Bw Kiarie aliamuru kesi hiyo ianze kusikizwa Desemba 19, 2013.
Bw Warui
alikuwa amepinga ombi la washukiwa hao Mabw Mohammed Ahmed Abdi, Liban
Abdullahi Omar, Adan Mohammed na Hussein Hassan Mustafah.
Wakili Mbugua
Mureithi anayewawakilisha washukiwa hao alimsihi hakimu mkuu katika
Mahakama ya Milimani Nairobi Waweru Kiarie Waweru , “ apewe muda wa siku
nane ndipo ajibu madai ya kiongozi wa mashtaka Warui Mungai kwamba
washukiwa hao watatoweka wakiachiliwa kwa dhamana.”
Bw Mureithi
alimweleza hakimu kwamba atawasilisha taarifa ya kiapo akisimulia
yaliyowafika washukiwa hao wakiwa korokoroni pamoja na “ masuala mengine
muhimu ya kisheria.”
Wakili huyo alisema anahitaji muda ndipo ajibu kila adai dhidi ya wateja wake kwa “ vile haki zao zimevunjwa.”
Bw Muriethi alisema “ hakupata muda wa kutosha kuwasiliana na jamaa za washtakiwa ndipo apate taarifa kamili kuwahusu.”
Alisema atamkabidhi Bw Mungai nakala ya taarifa atakayowasilisha kortini ndipo aijibu ikiwa atakuwa na jambo la kusema.
Wakili huyo
wa serikali (mungai ) alimweleza hakimu kwamba anahitaji muda wa siku
nne kujibu masuala ambayo yatasemwa na Mabw Abdi, Omar, Mohammed na
Mustafah.
Shtaka
Wanne hao
wanakabiliwa na shtaka la kushambulia duka la Westgate wakishirikiana na
magaidi wengine wa kundi la Al Shabaab mnamo Septemba 21, 2013 ambapo
watu zaidi ya 60 walikufa na wengi wakajeruhiwa.
Pia
washtakiwa hao wanadaiwa waliwaunga mkono magaidi Mohammed Abdinur
Said, Hassan Mohammed Dhohullow na wengine kutekeleza tendo la ugaidi
kwa kusababisha maafa katika duka la Westgate.
Mshukiwa
Mohammed Ibrahim anakabiliwa na shtaka la kumpa makao Abdikadir Hared
Mohammed ajulikanaye kwa jina jingine Mohammed Hussein akijua
ametekeleza tendo la ugaidi mnamo Oktoba 7.
Adan Mohammed
Ibrahim anakabiliwa na shtaka la kujiandikisha kama raia wa Kenya
ilhali ni raia wa Somalia. Anashtakiwa alijiandikisha katika kaunti ya
Mandera mnamo Julai 13, 2013.
Bw Ibrahim
anakabiliwa na shtaka la kupatikana nchini Kenya bila hati za kumwezesha
kukaa nchini Kenya ilhali ni raia wa Somalia.
Alikutwa na
maafisa wa idara ya uhamiaji katika Madrasa ya Salman Al-Faris katika
mtaa wa Eastleigh Nairobi mnamo Oktoba 14,2013.
Bw Hussein
Hassan Mustafa anakabiliwa na shtaka la kuwahifadhi magaidi Hassan
Mohammed Dhohullow na Mohammed Abdinur mnamo Septemba 21, 2013. Amekana
aliwahifadhi magaidi hao akishirikiana na watu wengine ambao
hawajafikishwa kortini.
