JELA MIAKA 10 KWA KOSA LA KUDANGANYA KUWA ALINAJISIWA

MWANAMKE amehukumiwa jela miaka 10 kwa kuwasilisha taarifa ya uongo katika kituo cha polisi cha Emali, Kaunti ya Makueni kwamba alikuwa amenajisiwa.
Afisa mkuu wa polisi wilayani Nzaui, Bw Kaburu  Manyala  alieleza kuwa mwanamke huyo alifika katika kituo hicho na kudai kuwa kuna mwanamume aliyekuwa amemnajisi.

Bw Manyala aliamrisha  maafisa wake  kumpeleka mama  huyo katika hospitali ya Makindu  kufanyiwa uchunguzi ambao ulithibitisha kwamba  alifanyiwa kitendo  hicho.

Mahakama ilifahamishwa kuwa mshukiwa aliyedaiwa alipokamatwa iligunduliwa kuwa, Kalumu Munyala, 21 hakuwa amenajisiwa kama alivyodai.

Mwanamume huyo alieleza kuwa alimtongoza mama  huyo na baada  ya kukubaliana  walienda na kukodisha  chumba  katika baa  moja  wakalala hadi asubuhi  na kumlipa Sh300 kabla ya kila mmoja kwenda zake.

Polisi pia walifanya uchunguzi katika lojing’i walikodaiwa kwenda ambapo mlinzi alithibitisha kuwapatia chumba.
Hatua hiyo ndiyo iliepelekea mwanamke huyo kufunguliwa mashtaka ya kutoa habari za uongo.

Onyo kali
Mwanamke huyo alikiri shtaka mbele ya Hakimu Mkuu wa Makindu, Bw Michael Kizito kabla ya kupokezwa kifungo cha miaka 10 jela bila faini.

Wakati huo huo, Bw Manyala  ametoa  onyo  kali kwa wanawake  wanaozurura  kituo cha biashara  cha  Emali  na kufanya   ukahaba  na  kuwatapeli wanaume pesa kwamba  watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Pia aliwatahadharisha wanaouza  bangi, dawa  za kulevya  na kunyonya  mafuta  ya dizeli  kutoka  kwenye  malori  ya  masafa marefu.

Uchunguzi uliofanywa  hivi punde  na wizara  ya  afya ni  kwamba  kituo  cha biashara  cha  Emali ni miongoni mwa  vituo  vya biashara  vinavyoongoza  kwa ugonjwa  hatari  wa Ukimwi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo