Marehemu Joseph Robert (Kushoto) Akiwa na wanafunzi wenzake waliomaliza mwaka wa tatu mwaka huu.
***
Taarifa zilizotufikia ni kwamba mpendwa huyo na mhitimu wa chuo kikuu
kishiriki cha SAUT - Tabora (AMUCTA) wa mwaka huu, aliyekuwa akisomea
kitivo cha elimu amefariki dunia katika maeneo ya machimbo karibu na
Geita hapo tarehe 27/10/2013 katika kutafuta maisha, na mwili
umepatikana jana tarehe 14/11/2013 huku ukiwa umeharibika sana na
kuzikwa mapema kijijini kwao huko Misungwi.
Marehemu alikuwa mtu wa watu, mpenda michezo na aliyeishi vizuri na wanachuo wenzake wa AMUCTA
*MUNGU AILAZE PAHALA PEMA ROHO YA MAREHEMU*
chanzo:aloyson.com