Mjadala Mkali waibuka kwenye Baraza la Madiwani Makete leo

Suala la asilimia 20 za mapato ya vijiji limeendelea kuwa gumzo katika baraza la madiwani katika halmashauri ya wilaya ya Makete kutokana na baadhi ya vijiji kutorejeshewa asilimia zao

Wakichangia hoja katika baraza hilo, baadhi ya madiwani akiwemo diwani wa Kinyika Mh Mwalyoyo na Mh. Beatrice Kyando wameonesha kusikitishwa na halmashauri kuchelewa kulipa asilimia 20 za vijiji licha ya maagizo kutolewa jambo walilodai linaleta sintofahamu katika kata zao
Madiwani wengine Mh Mwipelele Mbogela na Mh Asifiwe Luvanda wakaenda mbali zaidi na kutaka vikao vya madiwani visitishwe mpaka hapo asilimia 20 za vijiji zitakapolipwa huku Diwani wa Mlondwe Mh Alphonce akipinga mawazo hayo

Akitoa ufafanuzi wa hoja hiyo kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Makete Mwl. Gregory Emmanuel amekiri kuwepo kwa changamoto hiyo na kusema kwamba kinachopelekea ucheleweshaji huo ni pamoja na upunguaji wa mapato ya halmashauri jambo linalopelekea kiasi kidogo kinachopatikana kuelekezwa katika shughuli zingine zinazohitajika kuendesha halmashauri, huku akikiri kuwa agizo la baraza kutaka fedha zote za madeni ya asilimia 20 za vijiji zilipwe zote kabla ya Desemba 31 mwaka huu ni ngumu kutekelezeka

Baada ya majadiliano hayo Mwenyekiti wa halmashauri Mh Egnatio Mtawa akaagiza suala hilo lipelekwe kwenye kamati ya fedha kujadiliwa na kutoka na mkakati ambao hautaarhiri uendeshwaji wa shughuli za halmashauri

Sikiliza sauti jinsi ilivyokuwa kwa kubofya play>>>>>>


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo