
Rais Jakaya Kikwete amewatoa wasiwasi Watanzania wanaodhani kuwa
mchakato unaoendelea sasa kuhusu mafuta na gesi hautawanufaisha na
badala yake amesema serikali imejipanga vyema kuhakikisha taifa
linanufaika na rasilimali hizo.
Mh Rais ameyasema hayo katika uzinduzi wa awamu ya
nne ya ufunguaji wa zabuni za vitalu vya utafutaji wa leseni za
utafutwaji wa gesi na mafutra nchini.
Aidha Mh Rais amesema anatambua
mawazo mazuri yanayotolewa ya kuwashirikisha sekta binafsi Ili kuweza
nao kushiriki katika mchakato huo wa mafuta na gesi.
Pia kiongozi huyo mkuu wa nchi akaongeza kuwa kwa
sasa serikali inachofanya ni kuhakikisha kuwa inajenga uwezo wa kufanya
ukaguzi wa kina katika maeneo ambayo gesi .
Naye waziri wa nishati na madini Mh Profesa
Sospeter Muhongo amesema sera ya gaesi na mafuta Ipo tayari na
kichofanyika sasa ni kuiandika katika lugha ya Kiswahili.
Nao baadhi ya wabunge na wadau mbalimbvali
walioshiriki katika mkutano huo wamesema imekuwa jambo jema kwa rais
kutoa ufafanuzi wa jambo hilo kwa kina kutokana na ukweli kuwa watu
wengi walianza kuwa na wasi wasi kuwa taifa linapata hasara.