BREAKING NEWS: KITU KINACHOSADIKIKA KUWA NI BOMU CHATEGESHWA KANISA LA KIJITONYAMA

HILI NDILO KANISA LINALO DAIWA KUTEGESHWA KITU HICHO
Kinachoning'inia kwenye hiyo transfoma kinasadikiwa ni bomu...
Taarifa ambazo zimetufikia hivi punde kutoka kijitonyama jijini Dar es salaam zinasema kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania usharika wa Kijitonyama limenusurika kulipuliwa na kitu kinachodhaniwa kuwa ni bomu jioni hii baada ya watu wasiojulikana kutupa box lililofungwa huku ndani likiwa na kitu kinachodhaniwa kuwa ni wakati shughuli mbalimbali zikiwa zinaendelea.

shuhuda wetu kutoka eneo la tukio anasema box hilo limetupwa karibu kabisa na Transfoma ya TANESCO iliyopo ndani ya eneo la kanisa hilo.

wakati Tukio hilo likitokea shughuli mbali mbali zilikua zikiendelea kanisani humo ikiwa ni pamoja na mazoezi ya kwaya,Fellowship na maombezi ambapo waumini hao walistushwa na utupwaji wa box hilo kitendo kilichozua tafrani kubwa na kulazimika kuwasiliana na vyombo vya ulinzi na usalama ambapo vilifika eneo la tukio muda mfupi na kulichukua box hilo huku wakiwazuia waandishi wa habari kupiga picha box hilo.

Hata hivyo taarifa zinasema hakuna mtu yoyote ambaye amedhurika katika tukio hilo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo