Amiri jeshi mkuu Rais Jakaya Mrisho Kiwete ametoa onyo na agizo
hilo wakati akiwahutubia wananchi wa wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera
kwenye sherehe za kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya Kagoma
Rusaunga yenye urefu wa kilomita 154 inayojengwa kwa kiwango cha lami na
akafafanua kuwa operesheni hiyo itakayohusisha vyombo vyote vya ulinzi
na usalama itaanza wiki mbili zijazo katika mikoa ya Kagera, Geita na
Kigoma na ameonya kuhusu wahalifu hao watakaothubutu kuwafyatulia risasi
wanajeshi watakaokuwa kwenye operesheni hiyo.
Kuhusu barabara Rais Kikwete amesema serikali imedhamiria
kuiunganisha miji mikuu yote ya mikoa kwa barabara za lami chini ya
miradi mbalimbali ya barabara zinazojengwa kwa kiwango cha lami
inayotekelezwa kwenye mikoa mbalimbali nchini lakini akawahimiza
watanzania kuhusu umuhimu wa kuzitunza barabara hizo ili zidumu kwa
miaka mingi.
Katika hotuba yake ya utangulizi waziri wa ujenzi Dk John Magufuli
amesema barabara hiyo kutoka Kagoma Rusaunga imejengwa kwa gharama ya
zaidi ya shilingi bilioni 191 ikiwa ni fedha zinazotolewa na serikali ya
Tanzania ambapo mtendaji mkuu wa Tanroads injinia Patrick Mfugale
amesema kazi hiyo ambayo imeshakamilika kwa asilimia 96 inatarajiwa
kukamilika mwezi ujao.
Wakiongea kwenye mkutano huo baadhi ya mawaziri waliofuatana na
rais katika ziara hiyo wamezungumzia mipango ya serikali ya kuboresha
huduma za jamii kwa wananchi wa wilaya ya Biharamulo ikiwemo maji, umeme
na usafiri wa reli itakayopita hapo kutoka Isaka mpaka nchi za Rwanda
na Burundi.