MMOJA AUAWA KWA KUPIGWA RISASI KADHAA TEGETA DAR


Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Shabani Mrutu kwa mujibu wa vitambulisho vyake na mtumishi wa idara nyeti serikalini ameuwawa kwa kupigwa risasi tatu kifuani na watu wanaosadikika kuwa majambazi na kufariki papo hapo katika eneo la Magereji Tegeta kibaoni  jijini Dar es Salasam.
 
Tukio hilo lililovuta hisia za watu wengi limetoea majira ya mchana ambapo Bw. Mrutu alikuwa na gari lake namba T. 508 Ady akielekea magereji na kuvamia gafla na majambazi kwa kumiminiwa risasi muda mfupi baada ya kushuka.
 
Wekisimulia tukio hilo baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wamemwelezea marehemu kuwa alikutwa na mauti baada ya kujibizana na watu hao waliofika na pikipiki huku wakiulizana masuala yaliyowafanya kana kwamba wanafamiana na kisha kuchukua begi lake muda mfupi baada ya kummiminia risasi tatu kifuani.
 
Aidha upande wa mafundi gereji ambao walitaka kuficha majina yao walieleza kumzoea afisa huyo kwa kutengeneza magari yake eneo hilo ambapo hufika na maofisa wenzake kama ilivyokuwa leo ambao walitangulia kufika gereji na kutoweka baada ya tukio hilo huku mwenyekiti wa kamati ya ulinzi wa magereji hayo Muntazi Khan akieleza wasiwasi wa tukio hilo kuhusishwa na mgogoro wa magereji hayo na mwekezaji.
 
Kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi Kinondoni jijini Dar es Salaam Bw. Camilius Wambura aliyewahi kufika katika eneo la tukio kuungana na makachero wa jeshi hilo pamoja na kuomba ushirikiano wa walioshuhudia tukio hilo alikiri marehemu kuwa mtumishi wa serikali na kuahidi kuchukua hatua za haraka na kubaini wahusika na kuwafikisha katika vyombo vya sheria.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo