MTUHUMIWA WA UBAKAJI AKUTWA AMEKUFA GEREZANI


south_africa_serial_rapist
Mtu mmoja anayetuhumiwa kuwa mmoja wa wawabakaji wabaya zaidi nchini Afrika Kusini Sifiso Makhubo (pichani) amekutwa amekufa katika sero ya gereza alilokuwamo.

Sifiso Makhubo ambaye alikuwa anakabiliwa na mashitaka 122 likiwemo la mauaji, mwili wake umekutwa saa chache kabla ya kuanza kusikilizwa kwa kesi yake.

Pia alikuwa anashitakuwa kwa jaribio la kuua, kwa madai kuwa alikuwa akifahamu fika kuwa aliwaambukiza virusi vya ukimwi wale aliowabaka.

Afrika Kusini ina moja ya viwango vikubwa duniani vya matukio ya ubakaji, ambapo kwa mwaka uliopita kesi 64,000 ziliripoti polisi.

Pia ni nchi yenye idadi kubwa ya watu walioathirika kwa virusi vya ukimwi, ambapo watu milioni 5.5 sawa na asilimi 17 ya waathirika hao, wana umri kati ya miaka 15 hadi 49.

Mamlaka imesema Makhubo alikuwa mwenyewe katika sero hiyo na inaaminika alijinyonga kwa kutumia blanketi, hata hivyo wanachunguza mazingira ya kifo chake.

Alikuwa akishitakiwa kwa kuwabaka watoto 35 na wanawake wawili, kati ya Januari 2006 na Februari 2011, huku mhanga mdogo kabisa akiwa na umri wa miaka 10.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo