Mtu
mmoja anayetuhumiwa kuwa mmoja wa wawabakaji wabaya zaidi nchini Afrika
Kusini Sifiso Makhubo (pichani) amekutwa amekufa katika sero ya gereza
alilokuwamo.
Sifiso
Makhubo ambaye alikuwa anakabiliwa na mashitaka 122 likiwemo la mauaji,
mwili wake umekutwa saa chache kabla ya kuanza kusikilizwa kwa kesi
yake.
Pia
alikuwa anashitakuwa kwa jaribio la kuua, kwa madai kuwa alikuwa
akifahamu fika kuwa aliwaambukiza virusi vya ukimwi wale aliowabaka.
Afrika
Kusini ina moja ya viwango vikubwa duniani vya matukio ya ubakaji,
ambapo kwa mwaka uliopita kesi 64,000 ziliripoti polisi.
Pia
ni nchi yenye idadi kubwa ya watu walioathirika kwa virusi vya ukimwi,
ambapo watu milioni 5.5 sawa na asilimi 17 ya waathirika hao, wana umri
kati ya miaka 15 hadi 49.
Mamlaka
imesema Makhubo alikuwa mwenyewe katika sero hiyo na inaaminika
alijinyonga kwa kutumia blanketi, hata hivyo wanachunguza mazingira ya
kifo chake.
Alikuwa
akishitakiwa kwa kuwabaka watoto 35 na wanawake wawili, kati ya Januari
2006 na Februari 2011, huku mhanga mdogo kabisa akiwa na umri wa miaka
10.