MAMA SALMA KIKWETE KWENYE MAADHIMISHO YA MIAKA 40 YA JHPIEGO

Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,wama, Mama Salma Kikwete akipokewa rasmi na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Jhpiego nchini Tanzania, Bi Maryjane Lacoste kwenye hoteli ya Doubletree huko Masaki kulikofanyika sherehe ya kutimiza miaka 40 ya shirika hilo tarehe 23.4.2013.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipata maelezo kutoka kwa Dr. Maryrose Giattas, Cervical Cancer Prevention Program Adviser wa Shirika la Jhpiego kwenye maonyesho ya huduma mbalimbali zitolewazo na shirika hilo. Maonesho hayo yalifanyika katika hoteli ya Doubletree ikiwa ni sehemu ya kusherehekea miaka 40 ya shirika hilo.
Mama Salma Kikwete akipata maelezo kutoka kwa Dr. Hokororo wa shirika la JHPiego juu ya kuhifadhi vifaa vinavyotumika katika suala zima la afya ya mama na mtoto.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa na baadhi ya viongozi waliohudhuria sherehe ya kutimiza miaka 40 ya shirika la Jhpiego huko Doubletree hotel Masaki. Kulia kwa Mama Salma ni Dr. Leslie Mancuso, Rais na Mtendaji Mkuu wa Jhpiego akifuatiwa na Bi Sharon Cromer, Mkurugenzi wa Shirika la USAID nchini Tanzania. Kulia ni Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr. Seif Rashid akifuatiwa na Dr Allan Damiba, Jhpiego Senior Vice President na wa mwisho ni Mkuu wa wilaya ya Temeke Mheshimiwa Sophia Mjema, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo