Dina Marious aondoka Clouds Fm, sasa ni mtangazaji wa redio EFM

Aliyekuwa mtangazaji wa kipindi maarufu, Leo Tena cha Clouds FM, Dina Marious amejiunga rasmi na kituo cha redio cha EFM 93.7, Dar es Salaam.

Dina ametambulishwa rasmi Jumatatu hii sambaba na uzinduzi wa kampeni ya Muziki Mnene. Akizungumza na waandishi wa habari leo, Meneja Mkuu wa Mawasiliano wa EFM, Dennis Ssebo alisema kumpata Dina Marious kunawawezesha kuwapa wasikilizaji wao vipindi bora zaidi. 

“Katika kuhakikisha tunaendelea kukupa kilicho bora zaidi kupitia vipindi vyetu mbalimbali, sanjari ya kuwa na watangazaji mwenye ushawishi na uwezo mkubwa, leo hii tunamtambulisha kwenu mtangazaji Dina Marious ambaye wengi uwezo wake mnaujua. 

Na sasa ameungana na wenzake wenye uwezo mkubwa katika familia ya EFM. Dina atakuwa anatangaza kuanzia saa 8, 9, lakini bado hatujapanga vizuri, lolote linaweza kutokea,” alisema Ssebo. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo