Afisa biashara wilaya ya Makete Edonia Mahenge akisoma barua iliyotoka wizara ya TAMISEMI iliyoagiza kuwa wakusanye ada za leseni
Mia Kyando akichangia hoja katika mkutano huo
Mzunguko line akichangia
Mama Ipa Kyando akitoa hoja yake
========
Wafanyabiashara wa Makete mjini wameiomba serikali
kuangalia upya na kuwapunguzia gharama za leseni mpya ambazo kwa mujibu wa
sheria zinatakiwa zianze kulipiwa na wapate leseni mpya tangu Januari mosi
mwaka huu
Wamesema kutokana na ugumu wa biashara na mzunguko
mdogo wa hela uliopo wilayani Makete, inawawia vigumu kulipia fedha hizo ambapo
wameema kutokana na hali ngumu ya maisha gharama hizo zitazidi kuwaumiza
Wakizungumza kwenye kikao kati ya Afisa biashara
wilaya ya makete na wafanyabiashara hao kilichofanyika sokoni hapo, wamemtaka
afisa biashara kupeleka maombi yao kwenye ngazi husika kuwa wako tayari kulipia
ada ya leseni kila mwaka lakini wanaomba viwango vipungue
“Jamani hali ya wafanyabiashara hapa Makete ni ngumu,
mfano mzuri tangu tumeanza kufanya kikao hapa hakuna hata mteja mmoja aliyekuja
madukani mwetu kununua bidhaa, zaidi ya wanaopita ni wafanyabiashara wenzetu,
sasa tutapata wapi hayo malaki ya kulipia leseni” alisema Bw. Mia Kyando
Naye Mama Kathe ambaye pia ni mfanyabiashara sokoni
hapo amesema kuwa serikali imekurupuka kurudisha gharama za kulipia leseni kila
mwaka kwa kuwa hivi sasa muda umekwenda na tayari wananchi wanaishi kwa bajeti
na hivyo hili la sasa ni bajeti mpya ambayo itawaumiza
Akijibu hoja hizo Afisa biashara wilaya ya Makete Bw.
Edonia Mahenge amesema utaratibu huo umetoka wizarani hivyo wao kama
halmashauri hawana budi kutekeleza agizo hilo kama lilivyo
Amesema wanachukua mapendekezo yaliyotolewa na
wafanyabiashara hao lakini wakati wanayafikisha ngazi husika, zoezi la kulipia
leseni kwa mwaka huu litaendelea kama kawaida kwa kuwa wao wanatekeleza agizo
la barua ya TAMISEMI mpaka hapo watakapoambiwa vinginevyo
Bw. Mahenge amesema hawatamuonea wala kumkandamiza
mfanyabiashara yeyote, hivyo wafanyabiashara wote wanatakiwa kufika kwenye
ofisi ya biashara wilaya ya Makete ili kuanza kulipia na kupewa leseni mpya
ambazo zimeanza kutolewa tangu Januari mwaka huu, wakati ambapo wanasubiri
majibu ya mapendekezo waliyoyatoa