MWILI WA KATIBU MKUU KIONGOZI MSTAAFU MAREHEMU APIYO WAWASILI DAR

Baadhi ya maofisa wa Ikulu  wakiongozwa na aliyekuwa  Katibu Mkuu Kiongozi,  Philemoni Luhanjo (wa kwanza kushoto) wakiwa na sura za huzuni wakati wakiusubiri mwili wa marehemu Timoth Apiyo.
…Luhanjo akiambiwa jambo na mmoja wa wataalamu wa masuala ya Itifaki.
…  Baadhi ya waombolezaji waliofika kuupokea mwili huo kama wanavyoonekana pichani.
… Mkuu wa Wilaya ya Kionondoni, Jordan Lugimbana (wanne toka kulia) akiwa na baadhi ya maofisa wakati mwili ukitolewa ndani kuletwa nje ya uwanja wa ndege.
…Mwili wa marehemu Apiyo ukipokelewa.
…  Ukiombewa na waombolezaji.
… Ukiingizwa kwenye gari maalum ili upelekwe nyumbani kwake Sitakishari.
… Mwili ukiingizwa nyumbani Sitakishari.
…Waombolezaji wakilia mara baada ya mwili wa marehemu kufika nyumbani Sitakishari.

Ilikuwa ni simanzi kubwa ndani ya famila ya marehemu Timoth Apiyo pamoja na marafiki na viongozi wa serikali baada ya mwili wa katibu mkuu kiongozi mstaafu wa Ikulu kuwasili nchini ukitokea Afrika Kusini na kupokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere saa moja usiku jana .

Apiyo alikuwa katibu mkuu kiongozi enzi ya utawala wa awamu ya kwanza ya Mwalimu Julius Nyerere.

Katika mapokezi hayo, mkuu wa Itifaki kwenye mapokezi hayo ni aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu Philemon Luhanjo na mara baada ya kupokelewa mwili ulipelekwa nyumbani kwake Sitakishari, jijini Dar ambapo leo utaagwa katika Viwanja vya Karemjee na inatarajiwa Makamu  wa Rais  wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, Dk. Mohammed Bilal ndiye atakayeongoza zoezi hilo.

Baadaye mwili huo utapelekwa kuzikwa kwao kijijini Marasibora wilayani Tarime, Mkoa wa Mara.

PICHA, HABARI NA HARUNI SANCHAWA GPL


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo