MANDELA HOI, AKIMBIZWA TENA HOSPITALI


Nelson Mandela-1484223
Rais wa zamani wa Afrika Kusini Mzee Nelson Mandela amelazwa tena hospitali kutokana na kujirudia tena kwa ugonjwa wa mapafu.

Afya ya Mandela mwenye umri wa miaka 94 ilianza kudhoofika na kubidi kupelekwa katika hospitali mjini Pretoria, ambapo taarifa zimesema yuko katika hali mbaya lakini imara.

Msemaji wa rais nchini humo Mac Maharaj amekaririwa akisema baadhi ya wanafamilia wake wamekuwa na karibu muda wote.

Amesema ni hali ambayo amekuwa nayo kwa kipindi kirefu na wanamatumaini kuwa na sasa pia itatibika kwa mafanikio.

Katika taarifa yake kutoka ikulu amesema rais huyo wa zamani yuko chini ya uangalizi wa madaktari bingwa ambayo wananya kila liwezekanalo kuhakikisha anapata nafuu na kurejea katika hali ya kawaida.

Taarifa hiyo ya ikulu imeongeza kuwa Rais Jacob Zuma kwa niaba ya Serikali na taifa anamuombea Madiba apone haraka


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo