WAZIRI SITA AIPONDA RASIMU YA KATIBA MPYA

Waziri wa ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samweli Sitta amesema mchakato wa rasimu ya katiba mpya iliyotangazwa imelenga kuwatafutia ulaji viongozi wa serikali na kwamba inahitajika kufanyiwa kazi ya ziada na kudai kuwa muungano au shirikisho haviwezi kupatikana kama vipengele vinavyohusu serikali ya Tanzania bara havijaelezwa vizuri.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam kwenye mahafali ya chuo cha Ualimu Kibamba Mh Sitta amesema endapo kutakuwepo na rais wa Tanganyika ina maana nchi itakuwa kihoja kwa kuwa na marais watatu na kueleza kuwa kama yakipitishwa basi wananchi wakubali kuwepo na mzigo wa kuwahudumia na hata itifaki yake itakuwa ni tabu na kudai kuwa rasimu hiyo ni dhahiri viongozi wanajitafutia ulaji ndani ya katiba mpya kwani haelewi ni kwanini tume imependekeza mawaziri 15 wakati masuala ya muungano yapo saba


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo