SERIKALI KUFUNGA MACHIMBO YALIYOPOROMOKA ARUSHA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisaini kitabu cha Maombolezo baada ya watu kufukiwa na kifusi cha Moram na kufariki dunia jijini Arusha jana.

Serikali imetangaza kufunga machimbo ya Moram yaliyopo eneo la Moshono jijini Arusha mpaka itakapoweka utaratibu mzuri wa uchimbaji katika eneo hilo.

Waziri Mkuu nchini, Mizengo Pinda ametoa agizo hilo LEO baada ya kufanya ya kutembelea eneo hilo sanjari na kuwajulia hali majeruhi wawili walionusurika katika tukio hilo ambao wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru.

Pinda amefika LEO jijini Arusha majira ya mchana na kupokelewa na viongozi balimbali na kwenda moja kwa moja katika Hospitali ya Mt. Meru kuwatembelea majeruhi walionusurika katika ajali hiyo.

Katika hospitali hiyo Waziri Mkuu alishuhudia maiti 14 ambazo zilifukiwa na kifusi cha Moram na kutoa salamu za pole kwa ndugu wa wafiwa.

Baada ya kutoa salamu za pole kwa ndugu wa wafiwa msafara wa Waziri Mkuu ulielekea moja kwa moja katika eneo la tukio na kuona kifusi kilichowafukia watu hao na kusababisha kupoteza maisha.

Awali Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Stephen Masele ameueleza umma kwamba baadhi ya viongozi wa serikali na Halmashauri ya Jiji la Arusha kwamba wana tabia kuchukua mapato katika machimbo hayo badala ya kuangalia usalama kwanza wa wananchi.

“Viongozi wote wa serikali hapa Arusha pamoja na halmashauri ya jiji tusimamie usalama wa Watanzania kabla ya kukimbilia kupokea mapato,”amesema Masele.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo