MWANDISHI WA HABARI AVAMIWA NA MAJAMBAZI MOSHI

MWANDISHI wa Kampuni ya Tanzania Standard Newspapers (TSN) Limited inayochapisha magazeti ya Habari Leo, Daily News, na SpotiLeo, Peter Temba amevamiwa nyumbani kwake na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi, usiku wa kuamkia Aprili mosi mwaka huu.

Temba anayeandikia gazeti la Daily News mkoani Kilimanjaro, alisema alivamiwa saa 7:30 usiku katika kibanda chake cha kuuzia vinywaji na chakula kilichopo nyumbani kwake Rau Madukani wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro.

Alisema akiwa amepumzika ndani siku hiyo huku mkewe Yasinta Peter akiwa anafunga biashara yake, walifika watu watatu wakiwa na gari, ambayo haikutambulika, wakamkaba shingo mkewe wakitaka atoe fedha za mauzo. Mkewe aliomba msaada wamuachie ili aoneshe zilipo fedha za mauzo.

Hali hiyo ilisababisha dereva aliyekuwa akiendesha gari hilo kuliwasha na kukimbia huku akiwaacha wenzake wawili. Alisema wananchi walijitokeza na kukamata mtu mmoja kati ya hao na kumshambulia kwa silaha mbalimbali.
Polisi waliwasili eneo la tukio na kumnusuru mtuhumiwa huyo.

Alikimbizwa hospitalini lakini alifariki muda mfupi kabla ya kupatiwa huduma.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alithibitisha kuwepo tukio hilo.

Alisema mtuhumiwa huyo hajafahamika majina yake na mwili wake umehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Rufaa ya KCMC
CHANZO:HABARILEO


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo