Rais
wa Afrika Kusini Jacob Zuma alihudhuria misa mjini Pretoria kwa ajili
ya wanajeshi kumi na watatu wa nchi hiyo waliouwawa katika mapinduzi ya
serikali hivi majuzi katika Jamhuri ya Afrika ya kati.
Walifariki katika makabiliano na waasi karibu na mji mkuu Bangui.
Walifariki katika makabiliano na waasi karibu na mji mkuu Bangui.
Upinzani unataka uchunguzi rasmi wa madai hayo.
Zuma alisema kuwa wanajeshi hao walifariki wakiwa wanalinda amani na uthabiti wa bara la Afrika zaidi ya wiki moja iliyopita.
Wakati huo huo, Chama tawala cha ANC, kimekanusha madai ya uhusiano wa kibiashara na Jamuhuri ya Afrika ya Kati uliosababisha vifo vya wanajeshi wake 13.
Wanajeshi hao waliuwawa nchini humo mwezi jana wakati waasi walipouteka mji mkuu katika mapinduzi ya kijeshi yaliyomng'oa madarakani rais Francois Bozize.