Kufuatia hatua ya wizara ya mambo ya ndani kuwasimamisha kazi baadhi
ya maafisa wa jeshi la polisi wanaokabiliwa na tuhuma mbalimbali, jeshi
hilo limesema uchunguzi wa awali uliofanywa na mahakama ya kijeshi
umebaini kuwa askari hao wanahusika na tuhuma dhidi yao.
Baadhi ya tuhuma hizo ni pamoja na fedha zaidi ya Shilingi milioni
150, zilikamatwa eneo la Kariakoo jijini Dar es salaam na baadae kupotea
katika mazingira ya kutatanisha takribani miezi mitatu iliyopita .
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Kamanda wa jeshi la Polisi kanda maalum ya jijini Dar es salaam, Suleiman Kova amesema licha ya kusimamishwa kazi askari hao, watafikishwa mahakani wakati wowote.
Juzi waziri wa mambo ya ndani ya nchi Emanuel Nchimbi,
alieleza kuwa serikali haitasita kuwachukulia hatua za kinidhamu askari
yeyote atakayebainika kufunja sheria na kufanya kazi kinyume cha
maadili.