MKUU WA MKOA WA IRINGA ATOA SOMO KWA WAKULIMA


Katika kuhakikisha mkoa wa Iringa unajipanga vema kuondokana na baa la njaa linaloweza kujitokeza, Mkuu wa mkoa huo, Dokta Christina Ishengoma amewataka wakulima kutumia fursa za mvua zinazoendelea kunyesha kulima, kupalilia na kupanda mazao yanayostahimili ukame.

Akizungumza katika mkutano na wananchi wa kata ya Isimani, Dokta Ishengoma amesema kwa mwaka huu wa kilimo wa 2013 wakulima hawana budi kutumia vizuri hali ya hewa na mvua ambayo inaendelea kunyesha kwa kuwa karibu maeneo yote ya mkoa huo yameweza kufikiwa kikamilifu na mvua za kutosha.

Amesema kinachotakiwa kwa wakulima hao ni kuhakikisha mazao yao wanayapalilia, wanazingatia kilimo bora kwa mujibu wa mafunzo na maelekezo ya maofisa ughani ambao wametawanywa mkoa mzima.

Aidha, amewataka maofisa kilimo na ughani kuhakikisha wanakuwa karibu na wakulima na kutoa elimu kila wakati na badala ya kukaa maofisini na kusubiria kuitwa
SOURCE:EBONY FM


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo