FILAMU YA LOVE & POWER YA KANUMBA IPO TAYARI!.

Steven Kanumba
Marehemu Kanumba filamu yake ya mwisho kuigiza ya Love & Power

FILAMU ya Love & Power ambayo ndio kazi yake ya mwisho kuigizwa na msanii wa filamu nguli Bongo marehemu Steven kanumba inatarajiwa kuingia sokoni baada ya msambazaji wa filamu hiyo kuikamilisha na kusema kuwa filamu hiyo itanarajiwa kuingia sokoni mwezi wa nne, filamu ya Love & Power ni kazi ya kipekee kuigizwa na msanii huyo kabla ya umauti kumfika ni filamu aliyorekodi siku za mwisho kabisa.

Steven Kanumba
Marehemu Kanumba akiwa katika pozi.
Steven Kanumba
Filamu ya Love & Power ya marehemu Kanumba.
Steven Kanumba
Marehemu Kanumba akiwa katika pozi akivuta Siga.

Filamu hiyo pia ina historia ya kipekee kwani moja kati ya filamu iliyobeba wahusika wakubwa ambao ni marafiki wa marehemu Kanumba huku Daktari wa familia ya marehemu naye akiwa ameshiriki vema katika filamu hiyo.

Pengine ni filamu inayoweza kuibua hisia za watu wengi kufuatia filamu hiyo kuigizwa na wasanii watatu ambao kwa sasa ni marehemu, wasanii hao ni pamoja marehemu John Stephano, Hussein Mkiety ‘Sharomilionea’, lakini pia kuna msanii mwinge Irene Paul ambaye aliigiza kama mhusika mkuu, marehemu Kanumba alifariki mwaka jana mwezi wanne.

Msanii huyo anakumbukwa na wapenzi wa filamu kwa umahiri wake wa kuigiza na kuwa ni msanii pekee aliyeweza kuitangaza Tanzania kwa njia ya filamu na kuwa mmoja kati ya watu mashuhuri, filamu ya Love & power itasambazwa na Steps Entertainment ya jijini.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo