NAKWENDA KUPUMZIKA UARABUNI – WASTARA.


Wastara Juma
Stara mwigizaji wa filamu Swahiliwood.

MWIGIZAJI Nyota katika tasnia ya filamu Swahiliwood Wastara Juma ‘Stara’ amesema kuwa baada ya muda mwingi wa mihangaiko ya kuuguza na hata kumpoteza mumewe anahitaji kupumzika na kujenga akili upya, katika kulifanya hilo ameamua kwenda kupumzika Uarabuni kwa ajili ya kutuliza akili na kujipanga upya, akiongea na BLOG HII amesema kwa sasa anahitaji kupumzika kwa muda.

Wastara Juma
Stara akiwa na mtoto wake.
WastaraJuma
Stara akiwa katika pozi

“Nina safari wiki ijayo na kwenda Uarabuni kwa ajili ya kupumzika kisha baadae kuangalia nafanyaje kazi katika staili ipi, kwa sasa itakuwa ngumu kuwepo bila kufanya kazi lakini pia familia imeamua niende huko kama ni sehemu ya kunifariji zaidi kutokana na kipindi hiki kigumu,”anasema Stara.

Lakini mwanadada huyo asiye na makuu ameamua kwenda huko kupmzika kutokana na hali ya filamu ilivyo sasa ambapo watayarishaji wanajikuta wakikikaa kwa muda mrefu wakisotea kazi zao kutoka pasipo na wakati maalum, soko la filamu kwa sasa inasemekana ni gumu kuliko ambavyo jamii inaliona ukiona kazi imetoka sokoni ujue watu wametabika kwa kiwango kikubwa.
Wastara Juma.
Stara akiwa katika pozi.

Tunamtakia mapumziko mema na safari yenye Baraka na baadae akirudi arudi na nguvu mpya kwa ajili ya kuendeleza sanaa yetu Bongo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo