DC KYELA AIDANGANYA HALMASHAURI KUU YA CCM


Na  Ibrahim yassin, Kyela

KAMATI ya siasa ya Chama cha Mapinduzi CCM wilayani Kyela mkoani Mbeya imepinga taarifa ya utekelezaji wa Ilani iiyotekelezwa na serikali kwa kipindi cha miaka nane iliyowasilishwa na mkuu wa wilaya Kyela Magreth Malenga

Taarifa hiyo ilikuja kuwachefua wajumbe hao  baada ya Diwani wa kata ya Ikolo George Mwakabumbe kutaka kujua taarifa iliyosomwa ya maji kuwa hali ni nzuri wakati katika kata za Ikolo na Muungano wananchi wanakunywa maji machafu kwa kutokuwepo  maji salama ya bomba kwa zaidi ya miaka 20 mpaka sasa

Alisema taarifa iliyosomwa na mkuu huyo wa wilaya imepikwa tofauti na ukweli halisi uliopo katika maeneo ya vijiji na kata mbalimbali na kuhoji kuwa hajui taarifa hizi kazipata wapi wakati watu wanaugua homa za matumbo kutokana na watu kunywa maji machafu wanayoyachota kwenye mito ya Kiwira na Songwe

Msuli Mwaijengo mjumbe wa mkutano huo alisema kuwa hali ya maji wilayani ni janga la Kiwilaya na kuwa wilaya nzima  maji bado ni tatizo na kuwa taarifa hiyo ya mkuu wa wilaya imepikwa na kuwa mambo mengi ni ya uongo kama taarifa za mapagala,shule za awali zipo 99 wakati hakuna hata moja  na kuwa huo ni utani

Alisema  taarifa hiyo imekichefua Chama Cha Mapinduzi na kuwa anaiomba halmashauri hiyo ya CCM isiipokee kinyume cha hapo hakuna maendeleo ambayo yatafikiwa Kyela na kuwa hali hiyo inakipa ugumu chama hicho kujinadi kwa Wananchi

Cliford Mwaikinda  mwenyekiti wa kata ya Tenende,alikasirishwa na taarifa ya maendeleo ya elimu wakati elimu wilayani Kyela imeshuka kiasi cha kutisha na kuwa elimu ya msingi na ya sekondari  ni mbaya na kuwa taarifa zilizopo katika taarifa ya zinaonyesha kana kwamba ina matumaini wakati taarifa hiyo ni tofauti na uhalisia

Kaimu meneja wa mamlaka ya maji safi na maji taka Jorum Mkuyu alikiri wilaya kutokuwa na maji safi na kuwa hilo limetokana  na ukosefu wa fedha na fedha zenyewe ni msaada kutoka katika benki ya dunia ambazo bado hazijafika na kuwa kama hazitafika bado tatizo la maji litaendelea Kyela

Afisa mipango Clement Kasongo alisema kuwa hivi sasa kwa kuwa  fedha za benki ya dunia zimesimama wanatumia mapato ya ndani kuhakikisha kuwa wanafanya kwa sehemu kupunguza ukali wa tatizo la maji lililopo wilayani Kyela

Mkuu wa wilaya kwa upande wake alisema kuwa anashangaa kuona baadhi ya madiwani wanapingana na taarifa hiyo wakati katika vikao vya kamati walipitisha hoja hizo

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt,Hunter Mwakifuna alisema licha ya taarifa hiyo kuwa na mapungufu wameipitisha na kuwapa muda wa kujirekebisha kwa yale mapungufu yaliyojitokeza na kuwapa onyo watendaji kufanya vizuri kwenye miradi mbalimbali ili kukipa nafasi ya ushindi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo