ABDU KIBA AJIPANGA KUTOA VIDEO YA KIDELA


Na Elizabeth John

BAADA ya kutamba na kibao chake cha ‘Kidela’, mkali wa muziki wa kizazi kipya nchini, Abdukarim Kiba ‘Abdukiba’ amesema anajipanga kuandaa video ya kazi hiyo.
Mbali na ‘Kidela’ Abdukiba alishawahi kutamba na vibao vyake kama, Kizunguzungu, Demu sio na nyinginezo ambazo zilimtambulisha na kufanya vizuri katika tasnia ya muziki huo.
Akizungumza ijini Dar es Salaam, Abdukiba alisema kwasasa anatarajia kuanza kutengeneza video ya wimbo huo ambao amemshirikisha kaka yake ambaye pia ni nyota wa muziki huo, Alikiba.
“Namshukuru mungu kazi hii imepokelewa vizuri na mashabiki wangu nab ado inaendelea kufanya vizuri, naomba tu wapenzi wangu wasichoke kunipa sapoti bado kuna vitu vizuri ambavyo nimewaandalia,” alisema.
Abdukiba alisema, video hiyo atafanya na mtayarishaji maarufu nchini Adamu Juma, ambapo yeye ndio ataandaa mazingira ambayo watafanyia kazi hiyo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo