MATOKEO YA KIDATO CHA NNE HUWENDA YAKATANGAZWA KESHO

Dk Shukuru Kawambwa.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa amesema kwamba matokeo ya kidato cha nne yatatangazwa wiki hii kufuatia swali aliloulizwa kutaka kujua ni lini matokeo hayo yatatangazwa.

Dk Kawambwa alitangaza hilo pamoja na ajira mpya za walimu alipokutana na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam.

Kufuatia kauli ya Waziri huyo, inamaana sasa matokeo hayo yatatangazwa si zaidi ya kesho (Ijumaa) hasa kwa kuzingatia ukweli kwamba siku za kazi kwa ofisi za serikali zinaishia Ijumaa.

Alisema serikali haijachelewa kutangaza matokeo hayo kwani wanafunzi watajiunga na kidato cha tano Julai mwaka huu. “Hapo mtasema tumechelewa kivipi?


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo