JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI YATEKETEZA SILAHA HARAMU DAR ES SALAAM

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa 
Tanzania Dk. Mohammed Gharib Bilal (Katikati), 

akivuta kamba ikiwa ni  uteketezaji  wa silaha 

haramu katika Gereza la Ukonga Dar es Salaam leo. 

Kulia kwake ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani 

Perreira Silima na kushoto kwake ni Mkuu wa 

Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi Tanzania, 

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, (SACP), 

Simon Siro. Uteketezaji wa silaha hizo ulihusisha 

nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Silaha haramu zikiteketea baada ya kuchomwa moto. 
Imeelezwa kuna zaidi ya silaha haramu 500,000 

katika nchi zilizomo ndani ya 

Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Na Dotto Mwaibale

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Mohammed Gharib Bilal amesema mogogoro mbalimbali iliyopo katika za Jumuiya ya Mashariki inachangiwa na kuwepo kwa silaha haramu katika nchi hizo.

Hayo aliyasema Dar es Salaam leo katika zoezi la uteketezaji wa silaha haramu lililofanyika Ukonga Magereza na kuwashirikisha viongozi mbalimbali wa jumuiya hiyo.

"Takwimu zilizopo zimebaini kuwepo kwa silaha ndogo ndogo na kubwa ambazo hazimilikiwi kihalali na kusababisha kuwepo kwa matukio mengi ya kihalifu" alisema Bilal.

Alisema katika ukanda wa Afrika Mashariki takwimu zinaonesha kuna kuwepo kwa silaha haramu 500,000 hali inayoonesha kuwa kuna kazi kubwa katika kukabiliana na migogoro na aina mbalimbali za uhalifu katika jamii yetu.

Aliongeza kuwa katika ukanda huo kumekuwa na ongezeko la matukio ya kihalifu yanyotumia silaha na yamekuwa yakitokea maeneo ya mipakani na yale yanayohusisha muingiliano wa watu kutoka nchi moja kwenda nyingine.

Bilal alibainisha kuwa  matukio ya ujambazi, uvamizi na mengine ya aina hiyo yamekuwa yakiongezeka na chanzo chake ni kuwa na raia wasio waaminifu hasa wale wanaomiliki silaha haramu.

Alisema athari ya wazi  kabisa inayotokana na ongezeko la silahaaaa haramu ni ile inayojitokeza katika Sekta ya Utalii ambako tunashuhudia kuongezeka kwa matukio ya ujangili, ivamiziunaofanywa na maajangili katika mbuga za wanyama na kuhatarisha kwa kiasi kikubwa katika sekta hiyo.

Dk. Bilal alitumia fursa hiyo kuishukuru Serikali ya Ujerumani kupitia Balozi wake hapa nchini H.E. Klaus-Peter Brandes kwa kuisaidia jumuiya ya Afrika Mashariki kukabiliana na tatizo la silaha haramu kupitia shirika la Maendeleo la GIZ ambalo limesaidia kufanya zoezi hilo la kuteketeza silaha hizo.

"Nineambiwa kupitia ushirikiano kati ya Jumuiya yetu na GIZ masuala mbalimbali yamefanyika ambapo baadhi ya hayo ni kuijengea uwezo sekretarieti ya Jumuiya na nchi wanachama kwa kuratibu utekelezaji wa mpango wa kupambana na silaha haramu" alisema Dk. Bilal.

Dk. Bilal alizitaka nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kuungana katika kukabiliana na ongezeko la silaha haramu haraka iwezekavyo bila ya kusubiri kwani jukumu la ulinzi ni la nchi zote zilizopo ndani ya jumuiya hiyo.

Balozi wa Ujeruman nchini  H.E. Klaus-Peter Brandes, alisema matumizi ya silaha za maangamizi ni moja ya madhara ya mradi wa EA katika kukabiliana na SALW kwenye ukanda wa Afrika Mashariki ambao miaka sita iliyopita aliishauri sekretarieti ya Afrika Mashariki kukaa pamoja na serikali zao kuzungumzia suala hilo la kuzagaa kwa silaha hizo haramu.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo