MWANAFUNZI ACHINJWA KIKATILI NA KUNYOFOLEWA BAADHI YA VIUNGO


Na Ibrahim Yassin,Kyela

MWANAFUNZI wa darasa la sita katika shule ya msingi ya Kasumulu kata ya Ngana wilayani Kyela Kaselema Mpale (14) wa ameuawa kikatili kwa kuchinjwa na kisu kisha kunyofolewa baadhi ya viungo sehemu za mwili wake

Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi mama wa mtoto huyo Lucia Kamnyonge alisema kuwa tukio hilo lilitokea siku ya Ijumaa ambapo mnamo majira ya saa 10;30 baba yake alimtuma mtoto kwenda nyumba ya jirani kuchukua mpunga ambao ungetumika kama chakula cha siku hiyo

Alisema kuwa toka siku hiyo alipotumwa  mpunga akuweza kupatikanika hadi alipokutwa siku ya pili yake akiwa amekufa kwa kuchinjwa na kisu na na kunyofolewa baadhi ya sehemu zake za mwili ambazo ni Pua,mdomo,jicho ,kuondolewa sehemu zake za siri na kuchunwa ngozi ya kichwa karibu na utosi na mwili wake kutundikwa juu ya mti

Amefafanua kuwa baada ya hali hiyo kujitokeza taarifa ilipelekwa kwenye ofisi ya serikali ya kijiji ambapo uliitishwa mkutano wa wananchi wote wa kijiji hicho na ndipo wote walipotawanyika kuanza  kumtafuta mtoto huyo bila ya mafanikio baada baba yake alipomkuta mtoto huyo juu ya mti akiwa ametundikwa kichwa chini miguu juu na viungo vyake hivyo vikiwa vimenyofolewa

Mwenyekiti wa kitongoji cha Ibungumbati katika  kijiji hicho cha Ushrika lilipotokea tukio hilo ,Adamu Mkese alisema kuwa tukio hilo imeweza kuwashitua watu wa eneo hilo  na kuwa katika mkutano wa kijiji uliokaa kwa dharura wananchi walimuhusisha baba mzazi wa mtoto huyo ,Mpale Mbisa (35) kuhusika katika mauaji ya mtoto huyo

Alisema kuwa watu wa kijiji hicho wamemuhusisha baba wa mtoto huyo kutokana na mazingira ya kifo chenyewe na maelezo ya kujichanganya anayoyatoa baba huyo wa mtoto hasa jinsi yeye alivyomkuta mtoto huyo akiwa amekufa licha ya jamii ya watu wa eneo hilo kumtafuta mtoto huyo mchana na usiku bila ya kumuona na kushangazwa na taarifa kuwa yeye amemuona tena kiurahisi zaidi tena maeneo ambayo watu wote walipita kumtafuta mtoto huyo

Mwenyekiti huyo wa kitongoji  alisema kuwa katika mkutano huo wa kijiji mambo mengi yalizungumzwa na kuwa mzazi huyo wa mtoto alichukua fedha kwa mtu kiasi kama shs,milioni 7 ili kumuuza mtoto wake huyo ambapo alitekeeza azma hiyo na kulazimika kumkamata na kumpeleka polisi ambako bado anashikiriwa

Ofisa mtendaji wa kijiji hicho cha Ushirika ,Naomi  Charles alisema kuwa kuna dalili zote za baba huyo wa mtoto kuhusika  katika mauaji hayo kutokana na mazingira na kujichanganya kwa maelezo anayoyatoa na kuwa bado kuna watu wengine watatu ambao wanahusishwa na mauaji hayo na kuwa polisi wanaendelea na uchunguzi zaidi

Alisema  hisia hizo za wananchi zinaweza kuwa na ukweli ndani yake na kuwa jeshi la polisi linabidi kufanya uchunguzi wa kina na kuwa kama ataachiwa usalama wake utakua mdogo pale kijijini kutokana na watu walivyo na hasira naye kufuatia tukio hilo

Mwenyekiti wa kijiji hicho cha Ushirika Baruti Mwakasala alisema kuwa hari katika kijiji hicho si nzuri na kulishukuru jeshi la polisi kwa hatua za haraka walizozichukua na kuwa baada ya uchunguzi polisi waliruhusu mwili wa Mwanafunzi huyo kuzikwa

Alisema hisia za wananchi juu ya tukio hilo si za kubezwa na kuwa polisi wamepata pa kuanzia katka kufanya uchunguzi wao na kuwa ukweli utabainika tu

Ofisa tarafa wa tarafa ya Unyakyusa,Lwitiko Mwakalukwa alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwa yeye na mkuu wa wilaya walifika eneo la tukio na kujionea unyama huo na kutoa maagizo kwa jeshi  la polisi kufanya uchunguzi wa kina na wa haraka ili watu waliofanya kitendo hicho wabainike na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo