Imesemekana kuwa
tatizo lililopo wilaya ya Hanang’ Mkoania Manyara kwa upande wa boda
boda ni
elimu hawapewi kuhusu sheria za barabarani hivyo wanatakiwa kufuata
sheria na
kanuni za barabarani kuweza kupunguza vifo vya wanaboda boda.
Hayo yamesemwa na
mkuu wa polisi wilaya ya Hanang’ Arute Makita wakati akitoa maoni yake
kwenye
kikao cha watumishi wa idara mbalimbali kilichofanyika wilayani humo
mkoani
Manyara.
Aliongeza kuwa ili
kuweza kupunguza tatizo la ajali za waendesha pikipiki yaani boda boda
barabarani wamiliki wao pamoja na waajiri wao wanatakiwa kuwapeleka
shule ili
kuweza kupata elimu ya kutosha ili kuweza kupunguza vifo vya ajali
vinavyotokea
wakati wanapoendesha boda boda hizo.
Alibainisha kuwa
tangu mwezi wa sita mwaka jana mpaka sasa januari mwaka huu zaidi ya
watu 23
wamekufa kwa boda boda hivyo waendesha boda boda wanatakiwa kupatiwa
elimu ya
kutosha ili kuweza kupunguza vifo vya boda boda.
Naye mwakilishi
kutoka mahakama ambaye ni hakimu mhifadhi wilaya ya Hanang’ Saidi
Ding’ohi
amewataka watumishi nchini wafanye kazi kwa bidii na kuzingatia sheria
na
kanuni za kazi nakuweza kuzijua .
Pia amewataka
washiriki wa kikao hicho ambao ni watumishi wa idara mbali mbali
kuhudhuria
siku ya sheria itakayofanyika mwanzoni mwa mwezi wa pili nchini kote ili
kuweza
kujua kanuni na sheria za kazi.
Kwa upande wake
kutoka idara ya kilimo Afisa umwagiliaji Phineas Kasasi alisema kuwa ili
kuweza
kwenda mbele bajeti ya kilimo kuhusu pembejeo zinatakiwa ziwafikie kwa
wakti
wakulima na elimu inatakiwa itolewe ya kutosha kwa wakulima.
Aidha aliendela
kusema kuwa wanaofanya kazi watu wa vijijini wanatakiwa kupewa
kipaumbele pia
miradi mbali mbali imeingiliwa na wanasiasa ambapo wanataka wao
kuiongoza au
kuisimamia wao wametakiwa kuacha tabia hiyo.
