Imebainishwa kuwa
matukio ya ujangili kwenye Hifadhi ya Taifa ya Tarangire mkoani
Manyara
yamezidi kupungua kwani kwa muda wa miezi sita iliyopita hakukuwepo na
matuki
makubwa ya kuuawa tembo wa hifadhi hiyo.
Hayo yamebainishwa na
aliyekuwa mkuu wa hifadhi ya Tarangire Martin Loibooki ambaye hivi
sasa ni
mkurugenzi wa uhifadhi wa hifadhi za Taifa (Tanapa) wakati akizungumza
kwenye
tafrija ya kumuaga na kuukaribisha mwaka mpya iliyofanyika hifadhini
hapo
mkoani manyara.
Alibainisha kuwa hivi
sasa ujangili umepungua kwa kiasi kikubwa kwenye hifadhi hiyo ambayo
sehemu
yake kubwa ipo wilayani Babati mkoani Manyara na eneo la wilaya Kondoa
mkoani
Dodoma na wilayani Monduli mkoani Arusha.
Alisema kuwa ujangili
huo umepungukua kwa kiasi kikubwa kutokana na ushirikiano wanaopewa na
jamii
inayozunguka eneo hilo,askari wao na askari polisi kwani walifanikiwa
kukamata silaha mbalimbali ikiwemo bunduki kubwa na risasi.
Aliendelea kusema kuwa
wanashukuru hivi sasa mgogoro huo umefikia tamaki kwani mwenyekiti wa
kijiji
hicho na wananchi wake wametambua umuhimu wa hifadhi hii ya Taifa ya
Tarangire ambayo ni ya tatu kwa kuingiza mapato nchini.
Aidha alitaja miongoni
mwa changamoto zinazowakabili ni migogoro ya mipaka baina ya hifadhi
hiyo na
vijiji vinavyozunguka hifadhi hiyo ikiwemo kijiji cha Kimotorok cha
kata ya
Loiborsiret wilayani Simanjiro.
Kwa upande wake mkuu
wa mkoa wa Manyara Elaston Mbwilo alisema kuwa baadhi ya watu
wanaohujumu
hifadhi za Taifa kwa kufanya ujangili hawana uzalendo na hawatangulizi
maslahi ya Taifa kwani hifadhi zinaingiza fedha nyingi za kigeni.
Aliongeza kuwa kila mmoja kwa
nafasi yake ajitahidi kuboresha Hifadhi ya Taifa ya Tarangire ili
kuweza
kuongeza mapato kwani kwa asilimia kubwa mishahara ya watumishi
inatokana na
pato la utalii.
‘’Jamani fedha za
kuwalipa mishahara walimu,madaktari,askari wetu na watumishi wengine
wa
Serikali zinatokana na fedha zinazoingia kupitia utalii hivyo jamii
inapaswa
kutunza hifadhi ili hifadhi nazo zitutunze,” alisema mkuu wa mkoa wa
Manyara.
Alimalizia kwa
kusema kuwa ni lazima elimu itolewe kwa jamii kuhusu uhifadhi wa
wanyama pori
ili wawatunze na kuheshimu mipaka ambayo imewekwa sehemu ya hifadhi
ili
kuepuka hasara za kuharibu mipaka ya Tarangire.
