JOHARI AKANUSHA KUTOKA KIMAPENZI NA RAY


MSANII wa filamu Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’ amefunguka kuwa, licha ya watu kudai kuwa yeye ana uhusiano wa kimapenzi na msanii mwenzake Vincent Kigosi ‘Ray’, anaapa hawajawahi kufikia hatua hiyo.

Akizungumza kwa kujiamini, Johari ameweka  wazi   madai hayo ni  ya uongo na anashangaa kuona watu wanazidi kukomalia.

“Naapa sijawahi kulala na Ray. Nashangaa hizi habari zinavyozidi kuenea. Kwa hilo niko tayari kushika hata Biblia kuapia kuwa sina na wala sijawahi kuwa na uhusiano na Ray, uhusiano wetu ni wa kikazi tu,” alisema Johari.

Johari kwa muda mrefu amekuwa akidaiwa kutoka na Ray kwa siri lakini mwenyewe anakana huku wadau wakizidi kushikilia kuwa habari hizo zina ukweli ndani yake.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo