Tarehe 1 Disemba ya kila mwaka, jumuiya ya kimataifa huadhimisha siku ya UKIMWI duniani. Hii ni siku ya kutafakari kuhusu maisha yaliyopotea, na maisha yaliyobadilika milele kutokana na UKIMWI. Siku hii inatupa fursa ya kuwakumbuka zaidi ya watu milioni 34 wanaoishi na VVU duniani kote. Hali kadhalika, leo tunaadhimisha maisha yaliyookolewa na kuboreshwa nchini Tanzania na kukazia dhamira yetu ya kupambana na UKIMWI.
Aidha, tunatambua maendeleo makubwa yaliyofikiwa duniani katika kipindi cha miaka 30 iliyopita kutokana na tafiti mbalimbali na mbinu za kisayansi zinazotumika katika mapambano haya. Tarehe 23 Julai 2012, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Bibi. Clinton alitangaza kuwa Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na UKIMWI (PEPFAR) utaandaa mpango utakaoainisha awamu ijayo ya ushiriki wa Marekani katika jitihada za kimataifa za kukabiliana na UKIMWI. "Kwa upande wetu, mpango wa PEPFAR utaendelea kuwa kitovu cha utekelezaji wa azma yetu ya dhati ya kuona kuwa tunakuwa na kizazi kisicho na UKIMWI … Tungependa bunge letu lijalo la Congress, Waziri wetu wa Mambo ya Nje ajaye na wabia wetu wote wa hapa nyumbani na kote duniani wapate picha ya mambo yote tuliyojifunza na mpango utakaoonyesha mchango wetu katika kufikia azma ya kuwa na kizazi kisicho na UKIMWI,” alisema Bibi Clinton.
Mojawapo kati ya mambo tuliyojifunza ni kwamba sote tuna wajibu wa kushughulikia masuala ya kimataifa yanayohusu afya na kwamba hakuna nchi yoyote inayoweza kupambana na UKIMWI peke yake. Ili kufanikiwa katika mapambano hayo ni muhimu kwa nchi kufanya kazi na wabia kama vile PEPFAR na mashirika ya kimataifa kama Mfuko wa Kimataifa wa Kupambana na UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria (Global Fund). Kwa pamoja PEPFAR na Global Fund ziliwasaidia zaidi ya asilimia 70 ya watu wote walio katika matibabu ya kupunguza makali ya VVU/UKIMWI katika nchi zinazoendelea katika mwaka 2011.
Hapa Tanzania, ni lazima tuendelee kushirikiana katika kuongeza jitihada zetu dhidi ya VVU na UKIMWI. Kila mmoja wetu -- viongozi wa serikali, sekta binafsi, mashirika ya kimataifa, mashirika ya kiraia na mashirika ya kidini -- ana wajibu katika jitihada hizi. Hatua ya kuiwezesha nchi yenyewe kuchukua uongozi wa programu za kukabiliana na VVU/UKIMWI ni muhimu sana katika kuhakikisha uendelevu wa programu hizo.
Na Balozi Alfonso E. Lenhardt
Tarehe 1 Disemba ya kila mwaka, jumuiya ya kimataifa huadhimisha siku ya UKIMWI duniani. Hii ni siku ya kutafakari kuhusu maisha yaliyopotea, na maisha yaliyobadilika milele kutokana na UKIMWI. Siku hii inatupa fursa ya kuwakumbuka zaidi ya watu milioni 34 wanaoishi na VVU duniani kote. Hali kadhalika, leo tunaadhimisha maisha yaliyookolewa na kuboreshwa nchini Tanzania na kukazia dhamira yetu ya kupambana na UKIMWI.
Aidha, tunatambua maendeleo makubwa yaliyofikiwa duniani katika kipindi cha miaka 30 iliyopita kutokana na tafiti mbalimbali na mbinu za kisayansi zinazotumika katika mapambano haya. Tarehe 23 Julai 2012, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Bibi. Clinton alitangaza kuwa Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na UKIMWI (PEPFAR) utaandaa mpango utakaoainisha awamu ijayo ya ushiriki wa Marekani katika jitihada za kimataifa za kukabiliana na UKIMWI. "Kwa upande wetu, mpango wa PEPFAR utaendelea kuwa kitovu cha utekelezaji wa azma yetu ya dhati ya kuona kuwa tunakuwa na kizazi kisicho na UKIMWI … Tungependa bunge letu lijalo la Congress, Waziri wetu wa Mambo ya Nje ajaye na wabia wetu wote wa hapa nyumbani na kote duniani wapate picha ya mambo yote tuliyojifunza na mpango utakaoonyesha mchango wetu katika kufikia azma ya kuwa na kizazi kisicho na UKIMWI,” alisema Bibi Clinton.
Mojawapo kati ya mambo tuliyojifunza ni kwamba sote tuna wajibu wa kushughulikia masuala ya kimataifa yanayohusu afya na kwamba hakuna nchi yoyote inayoweza kupambana na UKIMWI peke yake. Ili kufanikiwa katika mapambano hayo ni muhimu kwa nchi kufanya kazi na wabia kama vile PEPFAR na mashirika ya kimataifa kama Mfuko wa Kimataifa wa Kupambana na UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria (Global Fund). Kwa pamoja PEPFAR na Global Fund ziliwasaidia zaidi ya asilimia 70 ya watu wote walio katika matibabu ya kupunguza makali ya VVU/UKIMWI katika nchi zinazoendelea katika mwaka 2011.
Hapa Tanzania, ni lazima tuendelee kushirikiana katika kuongeza jitihada zetu dhidi ya VVU na UKIMWI. Kila mmoja wetu -- viongozi wa serikali, sekta binafsi, mashirika ya kimataifa, mashirika ya kiraia na mashirika ya kidini -- ana wajibu katika jitihada hizi. Hatua ya kuiwezesha nchi yenyewe kuchukua uongozi wa programu za kukabiliana na VVU/UKIMWI ni muhimu sana katika kuhakikisha uendelevu wa programu hizo.
Kwa kupitia PEPFAR, Marekani itafanya kazi kwa karibu na Tanzania katika kujenga uwezo wake wa kuongoza, kutekeleza na hatimaye kubeba gharama zote za mapambano dhidi ya UKIMWI kwa kutumia fedha kutoka serikalini, mashirika huru ya kiraia na sekta binafsi ya Tanzania. Hii inaoana na Azimio la Abuja la Mwaka 2001 linalozitaka nchi wananchama wa Umoja wa Afrika kutenga angalau asilimia 15 ya bajeti zao za taifa kwa ajili ya sekta ya afya. Marekani imedhamiria kwa dhati kuendeleza ushirikiano wake na Tanzania inapoelekea katika kufikia azma hii.
Katika kipindi cha miezi 12 iliyopita, Tanzania imepiga hatua kubwa katika mapambano dhidi ya UKIMWI na Marekani ikiwa na fahari kubwa kusaidia jitihada hizo. Hivi sasa Marekani, kwa kupitia PEPFAR inatoa msaada wa dawa za kupunguza makali ya virusi vya UKIMWI kwa zaidi ya watu 364,000 - wanaume, wanawake na watoto.
Katika kipindi cha miezi 12 iliyopita, Tanzania imepiga hatua kubwa katika mapambano dhidi ya UKIMWI na Marekani ikiwa na fahari kubwa kusaidia jitihada hizo. Hivi sasa Marekani, kwa kupitia PEPFAR inatoa msaada wa dawa za kupunguza makali ya virusi vya UKIMWI kwa zaidi ya watu 364,000 - wanaume, wanawake na watoto.
Katika mwaka wa fedha 2012 pekee, PEPFAR kwa kupitia programu mbalimbali za utoaji matibabu, matunzo na ushauri nasaha iliweza kuwasaidia zaidi ya watu milioni 1.2 nchini Tanzania wakiwemo watoto yatima na walio katika mazingira magumu zaidi ya 526,000. Aidha, programu hizo zimewawezesha akinamama wajawazito milioni 1.1 kupata huduma ya upimaji wa VVU na ushauri nasaha kwa lengo la kuzuia maambukizi toka kwa mama kwenda kwa mtoto.
Mafanikio haya yanayodhihirishwa na maisha ya mamilioni ya watu yaliyookolewa ni makubwa, hata hivyo bado kuna kazi kubwa mbele yetu. Tunatumia maendeleo ya sayansi ili kuhakikisha kuwa tunatumia rasilimali tulizonazo kwa ufanisi na tija zaidi ili tuweze kupata matokeo makubwa zaidi na hivyo kuokoa maisha ya watu wengi zaidi. Mathalan, tafiti zinaonyesha kuwa tohara kwa wanaume inaweza kupunguza uwezekano wa maambukizi ya VVU kwa wanaume kwa zaidi ya asilimia 60.
Mafanikio haya yanayodhihirishwa na maisha ya mamilioni ya watu yaliyookolewa ni makubwa, hata hivyo bado kuna kazi kubwa mbele yetu. Tunatumia maendeleo ya sayansi ili kuhakikisha kuwa tunatumia rasilimali tulizonazo kwa ufanisi na tija zaidi ili tuweze kupata matokeo makubwa zaidi na hivyo kuokoa maisha ya watu wengi zaidi. Mathalan, tafiti zinaonyesha kuwa tohara kwa wanaume inaweza kupunguza uwezekano wa maambukizi ya VVU kwa wanaume kwa zaidi ya asilimia 60.
Kutokana na hali hiyo, PEPFAR katika miaka mitatu iliyopita imeongeza mara nane mchango wake katika programu ya kuhamasisha tohara ya hiari kwa wanaume nchini Tanzania. Eneo lingine muhimu ni lile la kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto ambapo PEPFAR imeweza kusaidia kutolewa kwa dawa za kuzuia maambukizi hayo kwa karibu asilimia 90 ya wanawake wajawazito waliobainika kuwa na VVU jambo ambalo limeweza kulinda afya ya mama na mtoto.
Tunapoangalia mbele, Marekani itaendelea kufanya kazi kwa karibu na Tanzania na wabia wake ili kuwa na mipango na shughuli za muda mrefu za kukabiliana na janga hili zitakazookoa maisha ya watu wengi zaidi. Katika kuadhimisha siku hii ya UKIMWI duniani, watu wa Marekani wanathibitisha tena dhamira yao ya dhati ya kushirikiana na Watanzania katika kufikia maono ya pamoja ya kuwa na Tanzania isiyo na VVU
Tunapoangalia mbele, Marekani itaendelea kufanya kazi kwa karibu na Tanzania na wabia wake ili kuwa na mipango na shughuli za muda mrefu za kukabiliana na janga hili zitakazookoa maisha ya watu wengi zaidi. Katika kuadhimisha siku hii ya UKIMWI duniani, watu wa Marekani wanathibitisha tena dhamira yao ya dhati ya kushirikiana na Watanzania katika kufikia maono ya pamoja ya kuwa na Tanzania isiyo na VVU