WATENDAJI WAZEMBE WA HALMASHAURI KUKIONA CHA MOTO

SERIKALI Wilayani  Rorya mkoani Mara imeonya kuwa haitasita kuwachukua hatua kali kwa watendaji katika halmashauri hiyo watakaoshindwa  kusimamia kikamilifu mapato ikiwa ni pamoja na kuhakikisha  fedha za miradi zinazotolewa inatekelezwa kwa wakati na kwa miradi ambayo imekusudiwa.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Rorya Bw Elias Goroi,katika kikao la kawaida cha baraza la madiwani amasema mapato ya halmashauri  hiyo yanapaswa kuongezeka  ili kuwa na uwezo wa kuhudumia miradi ya wananchi.

Amesema inasikitisha kuona kila mwaka  halmashauri hiyo inakubwa na dosari kubwa katika ukaguzi wa hesabu zake hivyo serikali sasa haitakuwa na huruma kwa wakuu wa idara watakaobainika  kuhusika katika matumizi mabaya  ya fedha za umma.
Ameongeza kuwa Halmashauri hiyo inapaswa  kuhakikisha  fedha zinazotolewa zinatumika vizuri na kwamba nidahamu itumike katika ukusanyanji wa mapato katika vyanzo vyote vya vya wilaya hiyo na kamwe wasisite kuwachukulia hatua wazabuni watakashindwa  kwenda na kasi hiyo.
Halmshauri ya Rorya kwa kipindi cha Julai 2011 hadi - Juni 2012  kupitia vyanzo vyake  imekusanya kiasi cha shlingi zaidi milioni 595.2 ikilinganishwa na makisio ya kukusanya  kukusanya kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 1.5  kwa kipindi hicho.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo